Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

Featured Image

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,

Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Violet Mumo (Guest) on April 20, 2017

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Richard Mulwa (Guest) on April 15, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Ann Wambui (Guest) on February 2, 2017

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Robert Ndunguru (Guest) on January 26, 2017

Katika imani, yote yanawezekana

David Sokoine (Guest) on November 24, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Mary Kidata (Guest) on November 4, 2016

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

David Kawawa (Guest) on October 31, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Alex Nakitare (Guest) on October 29, 2016

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Lydia Wanyama (Guest) on September 14, 2016

Rehema zake hudumu milele

Robert Okello (Guest) on August 25, 2016

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Violet Mumo (Guest) on August 24, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Elizabeth Mrema (Guest) on May 10, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Alex Nakitare (Guest) on April 7, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Joyce Mussa (Guest) on March 9, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Kenneth Murithi (Guest) on January 25, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Samuel Omondi (Guest) on December 17, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Mary Mrope (Guest) on November 30, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

John Lissu (Guest) on November 17, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Rose Amukowa (Guest) on October 20, 2015

Sifa kwa Bwana!

Lydia Wanyama (Guest) on September 26, 2015

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Joseph Njoroge (Guest) on August 29, 2015

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Alice Wanjiru (Guest) on August 18, 2015

Rehema hushinda hukumu

Simon Kiprono (Guest) on July 25, 2015

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Related Posts

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti T... Read More

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto... Read More

SALA YA IMANI

SALA YA IMANI

Mungu wangu,

nasadiki maneno yote linalosadiki na linalofundisha kanisa katoliki la Roma;Read More

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo ... Read More

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Read More
SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha ... Read More

AMRI ZA KANISA

AMRI ZA KANISA

1. HUDHURIA MISA TAKATIFU DOMINIKA NA SIKUKUU ZILZOAMRIWA

2. FUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJI... Read More

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.

Kwenye Msalaba Sali:

... Read More