Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Kisa cha kusisimua: Funzo kwa mabinti

Featured Image

Kijana maskini na mwenye maisha duni alimpenda msichana mmoja
Baada ya kutumia muda mwingi kumfikiria msichana huyo,
Siku moja akaamua kumwita na kumwambia ukweli ya kwamba amempenda na angehitaji kumuoa.

Msichana kwa nyodo na jeuri akasema "sikiliza tena unisikilize kwa makini wewe maskini mshahara wako unaopokea kwa mwezi hautoshi hata kwa matumizi yangu ya siku moja sasa utawezaje kunitunza mm!

Kwaufupi mm sio levo zako hivyo basi sahau kabisa kuhusu kunipata mimi
Nenda katafute maskini mwenzio atakae endana na maisha yako,
Mwisho akamwangalia kwa dharau na kisha akaenda zake.

Kwanzia siku ile kijana hakubahatika tena kumuona msichana yule lkn kwakuwa alimpenda basi hakuweza kumsahau kirahisi rahisi siku zilienda na miezi ikasonga,
Miaka 10 baadae wawili hawa walikuja kukutana katika supermarket moja hivi mjini

Kijana alipomwona msichana alitabasamu lakin kabla hajasema chochote msichana kama kawaida yake kwa dharau akasema "we maskin upo! hivi na ww unaingiaga supermarket eh!

Akaongeza huku akisema walau sasahivi nakuona umependeza inaonekana boss wako kakuongeza mshahara
ila kwa kifupi naomba nikwambie sasahivi nimeshaolewa mume wangu anafanya kazi kwenye kampuni moja hivi ya mtu binafsi kampuni maarufu sana na mshahara wa mume wangu ni shilingi milioni moja na laki mbili kwa mwezi na malupulupu mengine kibao,
Unafikiri ww na umaskini wako kuna siku utakuja kufikia kiwango cha mshahara anachopokea mume wangu!

Macho ya kijana yalitokwa na machozi kwa kuona msichana hajabadilika na anaendelea kuwa na maneno ya kejeri na dharau.

Mara hii mume wa yule dada akaingia ktk supermarket
Ile kumuona yule kijana mume akasema "ooh! Kiongozi upo hapa! Leo imekuwa bahati umekutana na mke wangu!" Kisha akamgeukia mke wake na kusema "mke wangu huyu ndo boss wangu

Na unajua nn mke wangu usishangae kumuona boss wangu anakuja kununua vitu mwenyewe hapa supermarket ukweli ni kwamba boss wangu hana mke, anasema alisha wahi kumpenda msichana mmoja lakini hakufanikiwa kumpata na amekuwa na ndoto ya kuja kukutana tena na msichana huyo ndio maana mpaka sasa bado hajaoa.

Akaendelea kusema hebu fikiria ni bahati kiasi gani alikuwa nayo msichana huyo kama angekubali kuolewa na boss wangu leo hii siangekuwa
maisha!

Muda wote msichana alikuwa kimya hajui hata ajibu nn kwa dharau alizomuonyesha kijana tangu mwanzo.


UJUMBE WANGU
Kwenye maisha mambo huweza kubadilika kama vile upepo unavoweza kubadili mwelekeo kulingana na masaa Hivyo basi usimdharau na kumbeza mtu yeyote kwa sababu ya hali aliyonayo,
Maana kila mtu anafungu lake alilopangiwa na Mungu,

Lakini pia kumbuka hakuna ajuaye kesho
Wakati mwingine mtu unayemdharau leo ndiye huyohuyo ambaye kesho utasimulia mafanikio yake.

Kwako unayesoma ujumbe huu nakuombea Mungu akakufungulie milango ya baraka na kuyapa thamani maisha yako ili pale ulipozomewa ukashangiliwe na wale wote waliokudharau punde wakapate kukupigia magoti kwa uweza wa Mungu.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Director J (User) on May 15, 2025

Good story πŸ’ͺ

Related Posts

Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu matakwa ya kiroho na imani ya mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kuheshimu matakwa ya kiroho na imani ya mpenzi wako

  1. Tambua Imani Yake Ni muhimu kujua imani ya mpenzi wako ili uelewe matakwa yake ya kiroh... Read More

Namna ya Kujenga Mahusiano ya Kujifunza na Kujua Mke Wako

Namna ya Kujenga Mahusiano ya Kujifunza na Kujua Mke Wako

Kujenga mahusiano ya kujifunza na kujua mke wako ni muhimu katika kukuza uhusiano wa karibu na kudum... Read More
Jinsi ya Kusimamia Vyema Majukumu katika Familia: Kuwa na Usawazishaji

Jinsi ya Kusimamia Vyema Majukumu katika Familia: Kuwa na Usawazishaji

Karibu sana katika makala hii inayojadili jinsi ya kusimamia vyema majukumu katika familia. Katik... Read More

Jinsi ya Kuwa na Ukaribu wa Kihisia na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Ukaribu wa Kihisia na Msichana

Kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na msichana ni jambo zuri sana. Hata hivyo, kuwa na ukaribu wa ... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kutokuwa na Msamaha katika Familia: Kuhamasisha Uwazi na Urejesho

Kukabiliana na Mazoea ya Kutokuwa na Msamaha katika Familia: Kuhamasisha Uwazi na Urejesho

Familia ni moja ya maeneo muhimu sana katika maisha ya mwanadamu. Hata hivyo, mara nyingi tunakab... Read More

Je, ni muhimu kuzungumzia kuhusu upendeleo wako wa ngono/kufanya mapenzi kabla ya kuingia katika uhusiano?

Je, ni muhimu kuzungumzia kuhusu upendeleo wako wa ngono/kufanya mapenzi kabla ya kuingia katika uhusiano?

Je, ni muhimu kuzungumzia upendeleo wako wa ngono kabla ya kuingia katika uhusiano? Jibu ni ndio!... Read More

Kufanya Mapenzi na Kuzeeka: Kufurahia Intimiteti katika Hatua Zote za Maisha

Kufanya Mapenzi na Kuzeeka: Kufurahia Intimiteti katika Hatua Zote za Maisha

Kufanya Mapenzi na Kuzeeka: Kufurahia Intimiteti katika Hatua Zote za Maisha

Kuna wakati m... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kusababisha Migogoro na Kuunda Amani na Furaha katika Familia

Kukabiliana na Mazoea ya Kusababisha Migogoro na Kuunda Amani na Furaha katika Familia

Katika familia, mazoea ya kusababisha migogoro ni kitu cha kawaida. Hata hivyo, ni muhimu kwa wan... Read More

Je, kuna mambo ya haramu katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna mambo ya haramu katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna mambo ya haramu katika ngono/kufanya mapenzi? Hili ni swali ambalo linaweza kuwa na maji... Read More

Jinsi ya kujua kama mwanamke anakupenda kweli kwa dhati

Jinsi ya kujua kama mwanamke anakupenda kweli kwa dhati

Yafuatayo ni maswali ya kujiuliza ili kujua kama mwanamke anakupenda kweli.

Anajitoa kwa ... Read More

Jinsi ya Kupata Msichana wa Kuwa na Uhusiano wa Mbali

Jinsi ya Kupata Msichana wa Kuwa na Uhusiano wa Mbali

Jinsi ya Kupata Msichana wa Kuwa na Uhusiano wa Mbali

Kuwa na uhusiano wa mbali sio rahisi... Read More

Kujifunza Mafanikio ya Kufanya Mapenzi ya Muda Mrefu: Sifa na Njia za Ushirikiano

Kujifunza Mafanikio ya Kufanya Mapenzi ya Muda Mrefu: Sifa na Njia za Ushirikiano

Kujifunza Mafanikio ya Kufanya Mapenzi ya Muda Mrefu: Sifa na Njia za Ushirikiano

Kufanya ... Read More