MAHITAJI
Unga – 3 Vikombe vya chai
Baking powder – 1 ½ Vijiko vya chai
Sukari – 1 Kikombe cha chai
Siagi – 1 Kikombe cha chai
Mayai – 2
Maji – kiasi ya kuchanganyia
Tende – 1 Kikombe
ufuta – ¼kikombe
MAPISHI
- Changanya unga, siagi, baking powder, na sukari katika bakuli
- Tia mayai, na maji kidogo uchanganye vizuri.
- Sukuma kiasi kama unavyosukuma chapati duara kubwa.
- Tandaza tende juu yake halafu kunja hadi mwisho.
- Paka mayai juu yake halafu mwagia ufuta kisha kata kata vipande.
- Vipange kwenye treya ya oveni kisha choma(bake)moto wa 350°F kwa muda wa nusu saa takriban.
- Ziepue katika moto naziache zipowe. Panga katika sahani.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE