Maisha ya ndoa yanahitaji maandalizi mazuri, kama waswahili wasemavyo nyote njema huonekana asubuhi, asubuhi ya maisha ya ndoa ni kipindi cha uchumba. Ndugu zangu, kipindi cha uchumba ni lazima tukitumie vizuri na kwa makini na kila jambo, ukitambua hakuna jambo dogo wa kubwa, kila jambo uliangalie katika mapana yake na katika uzito wake.
Hivyo basi huyo anayetaka kuwa na wewe jiulize maswali haya juu yake;
1. Je anamtambua Mungu na kuishi maisa ya kumpendeza Mungu, katika matendo yake na maneno yake?
2. Je huyo mchumba wako yupo tayari kukusaidia wewe kufikia malengo yako katika maisha?
3. Je huyo mchumba wako anakuheshimu na kukusikiliza au mtu anayekudharau?
4. Je mchumba wako anakushirikisha kila jambo kuhusu maisha yake na pia kuwa na utayari wa kupokea mawazo yako?
5. Je mchumba wako ana mawasiliano na wewe kwa kiasi kikubwa na kukujulia hali mara kwa mara?
6. Je mchumba wako yupo tayari kujitoa kwa ajili yako kwa hali na mali ili kufikia malengo yenu ya pamoja?
7. Je unatambua mazuri na mapungufu ya mchumba wako, hasa tukitambua hakuna mtu ambaye ni mkamilifu na namna gani mnasaidiana katika madhaifu yenu
8. Je mchumba wako ni msikivu au ni mtu ambaye anapoamua jambo ndilo analotaka hawezi kukusikiliza wala kupokea mapendekezo yako?
9. Je mchumba wako ni mwaminifu na anajitunza kwa ajili yako wewe tu au ni mtu ambaye haeleweki heleweki?
10. Je mchumba wako yupo tayari kukusamehe unapomkosea au kuomba msamaha anapokosea, au ni mtu mbishi
Haya ni mambo machache ambayo ni lazima kuyatafakari kuhu mchumba wako kama anakufaa kuunga naye NDOA? Usikurupuke.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Kuhamasisha Ushirikiano wa Kujifunza katika Familia: Kuweka Mwelekeo wa Kujenga Maarifa
Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Uwajibikaji na Kutozingatia Ahadi katika Familia Yako
Kuimarisha Uzoefu wa Kufanya Mapenzi: Jinsi Mawasiliano yanavyosaidia
Jinsi ya Kuendeleza Ushirikiano wa Timu katika Mahusiano
Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya usalama na ulinzi wa familia
Kuweka Kipaumbele cha Kujenga Nafasi ya Kujifunza na Kupata Maarifa katika Familia
Kuhamasisha Upendo na Kuonyesha Upendo katika Familia Yako
Jinsi ya Kuwa Mfano wa Uvumilivu na Uwazi katika Familia: Kujenga Uhusiano Thabiti