Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya

Mapishi ya Wali na kuku wa kienyeji

Mahitaji

Kuku wa kienyeji (boiler chicken 1)
Mchele (rice 1/2 kilo)
Nyanya ya kopo (tin tomato 1)
Vitunguu (onion 2)
Vitunguu swaum (garlic cloves 6)
Tangawizi (ginger)
Carry powder
Binzari ya njano (Turmaric 1/2)
Njegere(peas 1/2kikombe)
Carrot iliyokwanguliwa 1
Limao (lemon 1)
Bilinganya (aubergine 1)
Chumvi
Pilipili (scotch bonnet pepper)
Mafuta (vegetable oil)

Matayarisho

Loweka mchele kwa muda wa dakika 10 na uchuje maji yote kisha chemsha maji ya moto na uweke pembeni. Kisha tia mafuta kiasi katika sufuria na ukaange vitunguu, carrot na njegere pamoja. kwa muda wa dakika 5 baada ya hapo tia turmaric na chumvi. pika kwa muda wa dakika 5 na utie mchele na maji ya moto kiasi funika na upike mpaka uive.
Chemsha kuku pamoja na limao, chumvi, kitunguu swaum na tangawizi mpaka aive kisha mweke pembeni. Saga pamoja kitunguu,kitunguu swaum, tangawizi na nyanya. Kisha bandika jikoni na uache uchemke bila mafuta mpaka maji ya kauke.Baada ya hapo tia chumvi, mafuta ,curry powder, bilinganya na kuku. Kaanga pamoja kwa muda kisha tia maji au supu ya kuku kwa kukadiria mchuzi uutakao. Acha uchemke mpaka mabilinganya yaive na hapo mchuzi utakuwa tayari kuseviwa na wali.

Mapishi ya Kuku wa kukaanga

Mahitaji

Miguu ya kuku (chicken legs) 10
Kitunguu swaum na tangawizi (ginger & garlic paste) 1 kijiko cha chakula
Limao (lemon) 1
Pilipili iliyosagwa (ground scotch bonnet) 1/2
Giligilani iliyokatwakatwa (chopped coriander) kiasi
Chumvi (salt) kiasi
Mafuta ya kukaangia (veg oil)

Matayarisho

Safisha kuku kisha mtie kwenye sufuria na viungo vyote (kasoro mafuta na giligilani) kisha mchemshe mpaka aive na umkaushe supu yote. Baada ya hapo mkaange katika mafuta mpaka awe wa brown kisha mtoe na uweke katika kitchen towel ili kuchuja mafuta. Baada ya hapo weka katika sahani na umwagie giligilani kwa juu. Na hapo kuku wako atakuwa tayari kwa kuliwa.

Jinsi ya kupika Biskuti Ya Keki Kavu kwa kizungu Shortcake

Viamba upishi

Unga 2 Magi (vikombe vya chai)

Sukari iliyosagwa 2/3 Magi (kikombe cha chai)

Siagi   220 g

Unga wa mchele ½ Magi

Yai 1

Vanilla 1 kijiko cha chai

Jinsi ya kuandaa na kupika

1. Changanya vitu vyote hivyo kwenye bakuli mpaka unga ushikamane.

2. Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30 cm au (8 in kwa 12 in)

3. Choma kwenye moto 325˚C kwa muda wa saa nzima au mpaka ibadilike kuwa rangi ya dhahabu.

4. Epua acha ipoe kisha kata vipande kama mstatili, weak kwenye sahani tayari kunywewa na chai.

Jinsi ya kutengeneza Keki Ya Mbegu Za Mchicha

Viamba upishi

Unga ngano vikombc 3
Unga mbegu za mchicha kikombe 1
Baking powder vijiko vidogo
Maziwa kikombe 1
Sukari kikombe 1
Blue band kikombe ½
Mayai 10-12

Hatua

• Chagua, osha, kausha mbegu za mchicha mweupe, kisha saga zilainike.
• Chekecha unga wa ngano, unga wa mbegu za mchicha na baking powder Kwenye bakuli kubwa.
• Ongeza sukari na changanya.
• Ongeza mayai kidogo, kidogo ukikoroga na mwiko kwenda njia moja mpaka ilainike.
• Kama rojo ni zito ongeza mayai, au maziwa ili iwe laini, ongeza vanilla na koroga.
• Paka mafuta kwenye chombo cha kuoka au sufuria na chekechea unga kidogo.
• Mimina rojo ya keki na oka kwenye oveni au kama ni sufuria funika, weka moto mwingi juu, chini weka moto kidogo.
• Ukinusia harufu nzuri ya vanilla, funua, choma kisu katikati ya keki, kama ni kavu epua, pozesha na pakua kama kitafunio.

Mapishi ya Ndizi na Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Ndizi mbichi – 10-12

Nyama ng’ombe – 1 kilo moja

Kitunguu maji – 2

Nyanya/tungule – 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 7

Tangawizi mbichi – 1 kipande

Ndimu – 2 kamua

Chumvi – kiasi

Mafuta – 3 vijiko vya supu

Tui la nazi – 3 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Saga kitunguu thomu na tangawiz mbichi.
Weka nyama katika sufuria tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi na ndimu kisha chemsha hadi iive.
Menya ndizi ukatekate
Weka mafuta katika sufuria tia kitunguu maji kilokatwakatwa ukaange kidogo tu kisha tia nyanya/tungule uendelea kukaanga.
Tia tangawizi na thomu ilobakia.
Tia ndizi, kaanga kidogo kisha tia supu ya nyama na nyama yake.
Ziache ndizi ziive zikiwa tayari tia tui la nazi zikiwa tayari.

Upishi na Protini Ndogo: Kujenga Misuli na Kukaa Fiti

Upishi na Protini Ndogo: Kujenga Misuli na Kukaa Fiti 💪💪

Kuna njia nyingi za kuboresha afya yako na kuwa na mwili wenye nguvu na umbo zuri. Moja ya njia hizo ni kula vyakula vyenye protini ndogo. Protini ndogo ni nini? Hii ni aina ya protini ambayo ina molekuli ndogo na rahisi kumeng’enywa na mwili. Leo, kama AckySHINE, ningependa kushiriki nawe umuhimu wa upishi na protini ndogo katika kujenga misuli na kukaa fiti.

  1. Protini ndogo ni mchango muhimu katika kujenga misuli. Kwa sababu ya molekuli zake ndogo, protini hizi huingia haraka katika mfumo wa damu na kusaidia katika ukarabati na ujenzi wa tishu za misuli.

  2. Baadhi ya vyakula vyenye protini ndogo ni kama vile mayai, samaki, kuku, maziwa ya mbuzi, jibini la ng’ombe, na dagaa. Hivi vyote ni mfano mzuri wa vyakula ambavyo unaweza kula ili kuongeza kiwango cha protini ndogo mwilini mwako.

  3. Protini ndogo inasaidia pia katika kujenga misuli imara na yenye nguvu. Kama AckySHINE, nimeona athari chanya ya protini ndogo katika kuimarisha misuli yangu na kuongeza nguvu zangu wakati wa mazoezi.

  4. Kwa wale wanaotaka kujenga misuli au kubaki fiti, ni muhimu kula vyakula vyenye protini ndogo mara kwa mara. Hii inasaidia kutoa virutubisho muhimu mwilini na kuwezesha ukuaji wa misuli na ukarabati.

  5. Kumbuka kuwa kula vyakula vyenye protini ndogo pekee haitoshi. Ni muhimu pia kufanya mazoezi mara kwa mara na kula lishe yenye usawa ili kupata matokeo bora.

  6. Kwa wale ambao wanafanya mazoezi ya nguvu au michezo ya ushindani, protini ndogo inaweza kuwa sehemu muhimu ya lishe yao. Hii ni kwa sababu ya jukumu lake katika kujenga na kukarabati misuli baada ya mazoezi makali.

  7. Protini ndogo inaweza pia kusaidia katika kupunguza uzito. Kwa kuwa protini huchukua muda mrefu kumeng’enywa na mwili, husaidia kutoa hisia ya kushiba na kuwazuia watu kula sana.

  8. Ni muhimu kukumbuka kuwa kula protini ndogo kunapaswa kwenda sambamba na mazoezi na mtindo wa maisha wenye afya. Kwa hiyo, ni muhimu kuchanganya vyakula vyenye protini ndogo na mboga mboga, matunda, na wanga sahihi.

  9. Kama AckySHINE, napendekeza kula angalau gramu 0.8 za protini ndogo kwa kilo moja ya uzito wa mwili kwa siku. Hii inamaanisha kuwa mtu mwenye uzito wa kilo 70 anapaswa kula angalau gramu 56 za protini ndogo kwa siku.

  10. Kuna njia nyingi za kula vyakula vyenye protini ndogo. Unaweza kuchanganya mayai na mboga kwenye omelette au kula samaki pamoja na saladi ya mboga kama chakula cha mchana au chakula cha jioni.

  11. Kwa wale ambao ni mboga, unaweza kupata protini ndogo katika vyakula kama vile tofu, maharage ya soya, na njegere.

  12. Ni muhimu pia kutafuta ushauri wa kitaalamu kabla ya kuanza lishe yoyote mpya au kuongeza kiwango chako cha ulaji wa protini ndogo. Kwa kweli, unaweza kuwasiliana na mtaalamu wa lishe kukusaidia kutengeneza mpango bora wa lishe kulingana na mahitaji yako.

  13. Pia ni muhimu kukumbuka kuwa protini ndogo haipaswi kuchukua nafasi ya lishe yako yote. Ni sehemu tu ya lishe yenye usawa ambayo inapaswa kujumuisha pia wanga, mafuta yenye afya, na virutubisho vyote muhimu.

  14. Kumbuka kuwa kila mtu ana mahitaji tofauti ya lishe na viwango tofauti vya shughuli za mwili. Hivyo, ni muhimu kuzingatia mahitaji yako binafsi na kuzungumza na wataalamu kuhusu njia bora ya kudumisha afya na kuendelea kuwa fiti.

  15. Kwa hiyo, kama AckySHINE, nataka kutoa ushauri wangu kwa wote wanaotaka kujenga misuli na kukaa fiti: kula vyakula vyenye protini ndogo kwa kiasi sahihi, fanya mazoezi mara kwa mara, na kumbuka kuwa afya na ustawi wako ni muhimu sana.

Je, una maoni gani kuhusu upishi na protini ndogo? Je, umejaribu njia hii ya kujenga misuli na kukaa fiti? Tungependa kusikia kutoka kwako!

Mapishi ya viazi mbatata Vya Nazi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Mahitaji

Mbatata / viazi – 2 kilo

Nyama ng’ombe – ½ kilo

Kitunguu maji – 2

Tungule/nyanya – 2

Nazi /tui zito – 2 vikombe

Kitunguu saumu(thomu/galic) ilosagwa – 1 kijiko cha supu

Tangawizi mbichi ilosagwa – 1 kijiko cha supu

pilipili shamba/mbichi ilosagwa – kiasi

Mdalasini – 1 kipande

Bizari ya manjano – ½ kijiko cha chai

Bizari ya pilau/jiyrah/cummin – ½ kijiko cha chai

Ndimu/limau – 1

Namna Ya Kupika:

Chemsha nyama kwa kutia; chumvi, tangawizi, kitunguu thomu, mdalasini, na bizar zote.

Ipike nyama mpaka iwive na ibakishe supu yake kidogo.

Changanya tui la nazi pamoja na supu ilobakia.

Panga mbatata katika sufuria.

Tia nyama

Mwagia vitunguu na nyanya ulizotayarisha, tia pilipili.

Mwagia supu ulochanganya na tui

Funika upike mpaka viwive .

Tia ndimu

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo – 2lb

Nyanya – 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa – 1

Mafuta – 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi) – ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu – 1

Chumvi – Kiasi

Ndimu – Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa 400 gm

Nyanya 1

Kitunguu kilicho katwa 1

Nazi ya unga kiasi

Pilipili mbichi 2

Mafuta ½ kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika

Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa

Vipimo Vya Maharage

Maharage – 1 kopo

Kitunguu – 1

Nazi – 1 mug

Nyanya (itowe maganda) – 1 kiasi

Pilipili mbichi – 2

Mafuta – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.

Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi – 4/5

Kotmiri – 1 Kijiko cha supu

Ndimu – kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 chembe

Mafuta ya zaituni – 2 vijiko Vya supu

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha

Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali

Maji – 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe – 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.

Mawazo Mazuri ya Kifungua Kinywa cha Haraka na Salama kuanza Siku Yako Vizuri

Mawazo Mazuri ya Kifungua Kinywa cha Haraka na Salama kuanza Siku Yako Vizuri 🌅

Hakuna jambo bora zaidi kuliko kuanza siku yako vizuri na kifungua kinywa kinachokupa nishati na furaha. Kwa kuwa AckySHINE, ninapenda kushiriki nawe mawazo mazuri ya kifungua kinywa cha haraka na salama ambacho kitakusaidia kuanza siku yako vizuri. Hapa kuna orodha ya mawazo 15 ambayo unaweza kuyajumuisha katika maisha yako ya kila siku:

  1. 🍳 Chagua kifungua kinywa kinachojumuisha protini, wanga na mafuta yenye afya. Kwa mfano, unaweza kula mayai yaliyopikwa kwa mafuta kidogo na mkate wa ngano nzima.

  2. 🥣 Jumuisha nafaka nzima kama oatmeal au millet katika kifungua kinywa chako. Nafaka hizi zina nyuzinyuzi nyingi na zitasaidia kudumisha afya ya utumbo wako.

  3. 🍌 Ongeza matunda kwenye kifungua kinywa chako. Matunda yana virutubisho vingi na yatakupa nishati ya kutosha kwa siku yako.

  4. 🥛 Kinywaji cha maziwa kitakusaidia kupata protini na madini ya kalsiamu. Unaweza kunywa glasi ya maziwa ya mbuzi au kula jogoo au jibini la Cottage.

  5. 🍵 Kunywa kikombe cha chai ya kijani. Chai ya kijani ina antioxidants ambazo zinasaidia kuboresha afya ya moyo wako.

  6. 🥜 Ongeza karanga au mbegu kwenye kifungua kinywa chako. Karanga na mbegu zina mafuta yenye afya na omega-3 ambayo ni muhimu kwa afya ya ubongo wako.

  7. 🥗 Chagua kifungua kinywa kinachojumuisha mboga mboga. Unaweza kuongeza mboga kwenye omeleti yako au kula sahani ya saladi yenye mboga mbalimbali.

  8. 🍞 Ikiwa wewe ni mtu anayependa mkate, chagua mkate wa ngano nzima au mkate uliotengenezwa kwa unga mzima. Mkate huu una nyuzi nyingi na unakuweka kushiba kwa muda mrefu.

  9. 🍯 Ikiwa unataka kuongeza ladha tamu kwenye kifungua kinywa chako, tumia asali badala ya sukari. Asali ni afya na ina virutubisho vingi kuliko sukari iliyo na sukari nyingi.

  10. 🌿 Ongeza mdalasini kwenye kifungua kinywa chako. Mdalasini ina mali ya kupunguza sukari ya damu na inaweza kukusaidia kudhibiti hamu yako ya kula.

  11. 🥚 Ikiwa unapenda kula omeleti, hakikisha unatumia yai la kutosha na kuongeza mboga mboga zaidi. Hii itaongeza lishe na ladha ya chakula chako.

  12. 🥦 Jumuisha mboga kama broccoli kwenye kifungua kinywa chako. Broccoli ni tajiri na vitamini na madini na itasaidia kukuimarisha mfumo wako wa kinga.

  13. 🥤 Jaribu kinywaji cha smoothie kinachojumuisha matunda, mboga, na maziwa au maji. Smoothie itakupa nishati na virutubisho vingi.

  14. 🕙 Usikose mlo wa kifungua kinywa. Kula mlo wa kifungua kinywa ndani ya saa moja baada ya kuamka itasaidia kuamsha mwili wako na kuanza siku yako vizuri.

  15. 🍽️ Changanya vyakula tofauti katika kifungua kinywa chako ili uweze kufurahia ladha mbalimbali na kupata virutubisho vyote muhimu.

Kwa hivyo, kama AckySHINE, nakuomba ujaribu angalau moja ya mawazo haya ya kifungua kinywa. Utaona tofauti kubwa katika nishati yako na jinsi unavyohisi wakati wa siku. Kumbuka, kifungua kinywa ni muhimu sana na hakikisha unapata mlo kamili na lishe bora. Je, umeshajaribu njia yoyote ya kifungua kinywa ambayo imesaidia kuanza siku yako vizuri? Tuambie mawazo yako kwenye sehemu ya maoni hapa chini.

Mawazo Rahisi na yenye Afya ya Kujiandaa kwa Chakula cha Kazi

Mawazo Rahisi na yenye Afya ya Kujiandaa kwa Chakula cha Kazi

Kwa mara nyingine tena, hapa ni AckySHINE nikikuletea mawazo bora na yenye afya ya kujiandaa kwa chakula cha kazi. Kama unavyojua, chakula ni nishati muhimu katika kuwezesha utendaji wetu wa kazi. Kwa hiyo, ni muhimu sana kuwa na chakula bora na kilicho na lishe ili kuboresha ubora wa kazi zetu. Hapa kuna orodha ya mawazo 15 rahisi na yenye afya ya kujiandaa kwa chakula cha kazi:

  1. 🍎 Kula matunda na mboga safi kama tunda la kifungua kinywa. Matunda na mboga ni chanzo kikubwa cha vitamini na madini muhimu kwa afya yetu.

  2. 🍗 Chagua protini nzuri kama kuku, samaki au maharagwe kama sehemu ya chakula cha mchana. Protini ni muhimu kwa ukuaji na ukarabati wa misuli yetu.

  3. 🥦 Ongeza mboga za majani kama spinach na kale kwenye sahani yako. Mboga hizi zina virutubisho muhimu kama chuma na vitamini C.

  4. 🥪 Jenga sandwishi zenye afya kwa kutumia mkate wa ngano nzima, mboga mbalimbali na protini kama turkey au tofu. Hii itakupa nishati ya kutosha na kukusaidia kuhimili mawasiliano ya kazi yako.

  5. 🍓 Tumia matunda kama vitafunio vya asili. Matunda yana virutubisho na sukari asili ambayo ni bora kuliko pipi au vitafunio vya sukari.

  6. 🍅 Ongeza nyanya kwenye sahani zako. Nyanya zina lycophene, antioxidant ambayo inasaidia kulinda mwili dhidi ya magonjwa.

  7. 🍚 Chagua mchele wa kahawia badala ya mchele mweupe. Mchele wa kahawia una nyuzi nyingi na unaweza kukusaidia kusimamia uzito wako na kuboresha digestion yako.

  8. 🥛 Kunywa maziwa ya jamii ya skim au maziwa ya mbuzi badala ya maziwa ya ng’ombe ya kawaida. Maziwa ya mbuzi na maziwa ya jamii ya skim yana mafuta kidogo na yanaweza kusaidia kudumisha uzito wako.

  9. 🌽 Tumia nafaka nzima kama mkate wa ngano nzima, mchele wa kahawia au quinoa badala ya nafaka zilizopakuliwa. Nafaka hizi ni tajiri katika nyuzi na hutoa hisia ya kujazia kwa muda mrefu.

  10. 🥕 Ongeza karoti kwenye saladi yako. Karoti ni chanzo kikubwa cha vitamini A, ambayo inasaidia kuimarisha mfumo wetu wa kinga.

  11. 🍌 Kula ndizi kama chakula cha baada ya mazoezi. Ndimu zina wanga na potasiamu, ambayo inasaidia kuimarisha misuli na kurejesha nishati baada ya mazoezi.

  12. 🍚 Pika vyakula vyenye mafuta kidogo kama vile kukaanga kwa kutumia mafuta ya mizeituni. Mafuta ya mizeituni ni bora kwa afya ya moyo na yanaweza kusaidia kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.

  13. 🥤 Kunywa maji ya kutosha. Maji ni muhimu kwa afya na ustawi wetu. Unapaswa kunywa angalau glasi 8 za maji kwa siku.

  14. 🥦 Jaribu kuchemsha mboga zako badala ya kuzipika kwa muda mrefu. Kuchemsha mboga zitahifadhi virutubisho vyao na kuboresha ladha yao.

  15. 🥗 Jitahidi kula chakula kilichoandaliwa nyumbani na kuwa na udhibiti mkubwa juu ya viungo vyote unavyotumia. Hii inaweza kusaidia kuepuka vyakula vya haraka na kuongeza lishe kwenye chakula chako.

Hizi ni baadhi tu ya mawazo rahisi na yenye afya ambayo unaweza kuzingatia kujipatia chakula bora na kilicho na lishe wakati wa kukabiliana na changamoto za kazi. Kumbuka, chakula ni mafuta yetu ya ajabu ambayo inatuwezesha kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi. Kwa hiyo, kula vizuri na ujaze nishati yako! Je, una mawazo mengine yoyote kwa chakula cha kazi? Tafadhali shiriki nasi katika sehemu ya maoni hapa chini!

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Vipimo vya Wali:

Mchele – 3 vikombe

*Maji ya kupikia – 5 vikombe

*Kidonge cha supu – 1

Samli – 2 vijiko vya supu

Chumvi kiasi

Hiliki – 3 chembe

Bay leaf – 1

Vipimo Vya Kuku

Kidari (chicken breast) – 1Kilo

Kitunguu – 1

Tangawizi mbichi – ½ kipande

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 7 chembe

Pilipili mbichi – 3

Ndimu – 2

Pilipilimanga – 1 kijiko cha chai

Mdalasini – ½ kijiko cha chai

Jira/Cummin ya unga – 1 kijiko cha chai

Maji – ¼ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Wali:

Osha na roweka mchele kisha weka sufuria katika moto tia samli ipashe moto.
Tia hiliki, bay leaf, kaanga, kisha tia mchele ukaange kidogo.
Tia maji, chumvi na kidonge cha supu, upike wali kama unavyopika pilau.
*Maji kisia kwa kutegemea mchele ulivyo.
*Unaweza kutumia supu yoyote badala ya kidonge.

Kuku:

Katakata kidari cha kuku vipande vya kiasi, weka katika sufuria, tia ndimu, bizari zote, chumvi.
Katakata kitunguu vipande vidogodogo, pilipili, na kitunguu thomu (chopped), tia katika kuku.
Chuna tangawizi mbichi tia katika kuku. Changanya vitu vyote vizuri.
Tia maji kiasi ¼ kikombe tu kiasi cha kumkaushia kuku. Weka katika moto mpike huku unageuzageuza. Anapokaribia kukauka epua akiwa tayari kuliwa na wali (na saladi upendayo)

Jinsi ya kuandaa Muhogo, Samaki Wa Kuchoma Na Bamia

Mahitaji

Mihongo 3 – 4

Tui – 1000 ml

Chumvi – 1 kijiko cha chai

Kitunguu maji kilokatwakatwa – 1

Nyanya mshumaa – 3-4

Pilipili mbichi ndefu – 2-3

Pilipili boga – 2

Namna Ya Kutayrisha Na Kupika

Menya mihogo kisha ikate kate vipande inchi tatu hadi nne, kila kipande kigawe kitoke vipanda vinne. Toa mzizi katikati
Osha mihogo ipange kwenye sufuria ya nafasi na yenye mfiniko, ili upate nafasi ya kutia viungo unavyoona pichani na utokotaji wa tui wahitaji nafasi.
Panga/tandaza kitunguu, nyanya mshumaa/tungule,pilipili mbichi na pilipili boga juu ya mihogo, tia chumvi na tui lote.
Funika sufuria kisha weka jikoni moto wa kiasi kuchemsha tui lipande juu. Hakikisha tui halifuriki na kumwagika kwa kuchungulia au kufunika nusu mfuniko
Kwa mda wa nusu saa hivi ukiona sasa tui linatokota chini chini fuinika mfiniko na upunguze moto mdogo kabisa tui likauke kidogo na liwe zito.
Toa muhogo moja ubonyeze ukiona umewiva zima jiko na wacha sufuria hapo kwa muda wa 10. Mihogo tayari kuliwa.

Kidokezo.

Tui lote huwa chini baada ya mihogo kuwiva unapopakuwa teka kutoka chini uweze kupata uzito wa tui umwagie juu.

Bamia/Mabenda

Bamia – robo kilo

Nyanya – 3

Kitunguu maji – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au ilosagwa – 1 kijiko cha chai

Nyanya kopo (tomato paste) – 1 kijiko cha supu

Mafuta – 150 ml

Chumvi -1 kijiko cha chai

Pilipili boga – 1

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Kata vichwa vya bamia kisha zikate kate mara mbili zikiwa kubwa, ikiwa ni ndogo mno haina lazima kuzikata osha tu uweke kando.
Katika sufuria, katakata kitunguu, nyanya, pilipili boga tia ndani viungo hivi ongeza chumvi mafuta, thomu na nyanya kop
Washa moto mdogo mdogo huku umefunika sufuria kwa muda wa dakika 20 kisha ukiona mboga zimeshika kutokota ongeza bamia koroga.
Tia maji 200ml wacha kwa muda wa dakika 15 kupikika tena, ukionja utamu wa mboga na chumvi, hakikisha bamia pia zimewiva. Tayari kuliwa.

Samaki Wa Kuchoma

Samaki (dorado) au mikizi au una – 2 wakubwa (fresh)

Chumvi – 1 kijiko cha chai

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au iliyosagwa 1 ½ cha chai

Tangawizi mbichi iliyosagwa – 1 kijiko cha supu

Namna Ya Kutayrisha Na Kuchoma

Safisha samaki vizuri mchane chane (slit) kwa ajili ya kuweka masala.
Changanya viungo vyote na chumvi samaki kisha paka katika samaki kote na ndani ya sehemu ulizochanachana. Mroweke kwa muda wa robo saa hivi.
Weka karatasi ya jalbosi (foil paper) katika treya ya oveni. Muweke samaki kisha mpike (grill) kwa moto wa juu achomeke hadi samaki agueke rangi na awive.

Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu

MAHITAJI

Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) – vikombe 2

Maziwa ya Mgando Matamu ya Kopo – 2 vikombe

Nazi iliyokunwa – ½ Kikombe

Chokoleti vipande vipande – 1 Kikombe

Njugu vipande vipande – ½ Kikombe

Siagi – 227 g

MAPISHI

Yeyusha siagi motoni kisha changanya na unga wa wafer acha kidogo motoni
Mimina katika treya unayochomea itandaze vizuri, kisha mimina maziwa juu yake pamoja na njugu vipande , nazi iliyokunwa na vipande vya chokoleti.
Choma (bake) kwenye oveni kwa moto wa 350ºC kwa dakika 20.
Katakata tayari kwa kuliwa

Jinsi ya kutengeneza Bisikuti Za Kaukau Na Kahawa (Cocoa Coffee Biscuits)

MAHITAJI

Maji baridi – kikombe 1

Biskuti za kawaida – paketi 2

Kaukau (cocoa) – vijiko 3 vya kulia

Kahawa ya unga – kijiko 1 cha kulia

Njugu mchanganyiko zilokatwakatwa – kikombe 1

Sukari – kiasi upendavyo

MAANDALIZI

Changanya maji na kaukau na kofi na sukari
Katakata biskuti kisha tia paketi moja na nusu uchanganye vizuri.
Kisha nusu ya biskuti zilobakia katakata vipande vikubwa na weka juu ya mchanganyiko, kisha changanya kidogo tu.
Weka katika foil paper na zungusha (roll)
Kisha fungua umwagie njugu au mkassaraat zilosagwa
Kisha roll katika foil paper na uweke katika freezer mpaka igande
Kisha kata kata slices na iko tayari

Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga

Vipimo

Wali:

Mchele mpunga – 4 Vikombe

Tui la nazi – 6 vikombe

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele weka kando.
Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.
Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.

Maharage Ya Nazi

Maharage – 3 vikombe

Tui la nazi zito – 1 kikombe

Tui la nazi jepesi – 1 kikombe

Kitunguu maji – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa -1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Chemsha maharage mpaka yaive.
Katiakatia kitunguu maji na tia thomu, tia na tui jepesi kikombe kimoja.
Tia tui zito endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi yakaribie kukauka yakiwa tayari.

Samaki Nguru Wa Kukaanga

Samaki Wa Nguru – 4 vipande

Kitunguu saumu(thomu/galic) & tangawizi ilosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi – 4

Ndimu – 2 kamua

Bizari ya samaki -1 kijiko cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki.
Mwache akolee viungo kwa muda kidogo.
Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.

Mapishi ya Mihogo ya nazi na kuku

Mahitaji

Mihogo kilo 1
Kidali cha kuku 1 kikubwa
Nyanya 1 kubwa
Kitunguu maji 1 cha wastani
Swaum/tangawizi i kijiko cha chai
Nazi kopo 1
curry powder 1 kijiko cha chai
Binzari manjano 1/2 kijiko cha chai
Limao 1/2
Pilipili 1
Chumvi kiasi

Matayarisho

Saga pamoja nyanya, kitunguu na swaum/ginger pamoja na vimaji kidogo. Kisha vitie kwenye sufuria isiyoshika chini na uvishemshe mpaka maji yote yakauke kisha tia mafuta na upike ktk moto mdogo mpaka viive.Baada ya hapo tia spice na uzipike kidogo kisha tia mihogo na kuku (kuku na mihogo vikatwe vipande vya wastani) vichanganye vizuri kisha tia nazi na vimaji kiasi,limao chumvi na pilipili na ufunike kisha punguza moto. Pika mpaka mihogo na kuku viive na ibaki rojo kidogo kisha ipua na mihogo yako itakuwa tayari kwa kuliwa

Mapishi ya Pilau Ya Mchicha

VIPIMO

Mchele – 3 Vikombe

Mchicha

Mafuta – 1/2 kikombe

Vitunguu maji – 2 vikubwa

Nyanya – 1

Viazi – 3

Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa – 3 vijiko vya supu

Vidonge vya supu (Stock cubes) – 3

Jiyrah (cummin powder) – 1 kijiko cha chai

Pilipili manga ya unga – 1 kijiko cha chai

Hiliki ya unga – 1/2 kijiko cha chai

Mdalasini – 1 kijiti

Maji (inategemea mchele) – 5 vikombe

Chumvi

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

1. Osha na roweka mchele.

2. Osha mchicha, chuja maji na katakata.

3. Katakata vitunguu maji, nyanya.

4. Menya na kata viazi vipande ukaange pekee vitoe weka kando.

5. Katika sufuria tia mafuta na kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi.

6. Tia thomu, bizari zote, kaanga kidogo kisha nyanya.

7. Tia mchicha kaanga kidogo kisha tia mchele, maji na vidonge vya supu, chumvi.

8. Koroga kidogo kisha tia viazi ulivyovikaanga, funika na acha uchemke kidogo katika moto mdogo mdogo.

9. Kabla ya kukauka maji, mimina katika chombo cha kupikia ndani ya oven (oven proof) au katika treya za foil, funika vizuri na upike ndani ya oven moto wa 400º kwa dakika 15-20 upikike hadi uive.

10. Ukishaiva epua na tayari kuliwa na kitoweo chochote upendacho.

Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng’ombe

Vipimo

Ndizi mbichi – 10

Nyama – kilo 1

Nazi ya kopo – 1

Chumvi – 1 Kijiko cha chakula

Ndimu – 1

Bizari ya manjano – 1 Kijiko cha chai

Pili pili mbichi – 3

Nyanya (tomatoes) – 2

Kitunguu maji – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi iliyosagwa – 1 Kijiko cha chakula

Namna ya Kutayarisha Na Kupika

Kata nyama vipande vipande na uisafishe.
Chemsha nyama weka chumvi, thomu, tangawizi na ndimu. Iache iwive.
Kata kata nyanya na kitunguu, kisha mimina kwenye nyama inayochemka, weka na bizari nusu kijiko. Wacha supu iwive kisha weka pembeni. Ukumbusho: Hakikisha supu inakuwa kiasi na si nyingi.
Menya maganda ndizi na uzikate vipande vipande vya kiasi.
Zikoshe ndizi na uziweke ndani ya sufuria.
Weka maji ndani ya sufuria kisha zichemshe ndizi mpaka ziwe laini kidogo.
Zimwage maji ndizi kisha mimina supu na nyama ndani ya ndizi.
Mimina nazi pili pili na bizari nusu kijiko ndani ya ndizi na uziweke kwenye jiko zichemke mpaka zibakie na urojo kiasi. Onja chumvi na uongeze kadri utakavyopenda.
Weka pembeni zipoe.
Pakua ndizi kwenye sahani au bakuli tayari kwa kuliwa.

Upishi na Matunda ya Mzabibu: Vitamu vyenye Antioxidants

Upishi na Matunda ya Mzabibu: Vitamu vyenye Antioxidants 🍇

Habari za leo wapenzi wa chakula na afya! Leo nataka kuzungumzia faida ya upishi na matunda ya mzabibu. Kwa mujibu wa utafiti wa hivi karibuni, matunda haya matamu yanajulikana kuwa na virutubisho na antioxidants nyingi ambazo zinaweza kuleta manufaa makubwa kwa afya yetu. Kama AckySHINE, nina ushauri muhimu na maelezo kuhusu jinsi ya kufurahia vitu hivi vyenye faida ya ajabu. Soma makala hii ili kujua zaidi!

  1. 🍇 Faida ya kwanza ya matunda ya mzabibu ni kwamba yana antioxidants nyingi ambazo husaidia kupambana na athari za radicals huru katika mwili wetu. Hii husaidia kulinda seli zetu dhidi ya uharibifu na kuimarisha mfumo wetu wa kinga.

  2. 🍇 Kula matunda ya mzabibu kunaweza kusaidia kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo. Antioxidants zilizopo katika matunda haya husaidia kupunguza viwango vya cholesterol mbaya na kuboresha afya ya moyo.

  3. 🍇 Matunda ya mzabibu yana kiwango kizuri cha vitamini C, ambayo ni muhimu kwa afya ya ngozi yetu. Vitamini C husaidia kujenga collagen, ambayo ina jukumu kubwa katika kuifanya ngozi yetu ionekane nzuri na yenye afya.

  4. 🍇 Kwa kuwa na kiwango cha juu cha maji, matunda ya mzabibu yanaweza kusaidia katika kudumisha afya ya figo. Maji ya kutosha mwilini ni muhimu kwa kazi nzuri ya figo.

  5. 🍇 Pia, matunda haya yana kiwango kikubwa cha resveratrol, ambayo inajulikana kwa uwezo wake wa kupambana na uchochezi. Hii inaweza kuwa na manufaa sana kwa watu wenye matatizo ya uchochezi kama vile ugonjwa wa arthritis.

  6. 🍇 Kwa kuwa ni chanzo kizuri cha nyuzi za chakula, kula matunda ya mzabibu kunaweza kusaidia katika kudumisha afya njema ya utumbo wetu. Nyuzi hizi husaidia katika kuzuia matatizo ya kuvuja kwa utumbo na kuboresha mwendo wa utumbo.

  7. 🍇 Je, umewahi kusikia kuhusu mafuta ya mbegu za mzabibu? Mafuta haya yana virutubisho muhimu kama vile asidi ya linoleiki na vitamini E ambavyo husaidia kulinda ngozi yetu dhidi ya madhara ya mazingira na kuifanya iwe laini na yenye afya.

  8. 🍇 Kulingana na utafiti, matunda ya mzabibu yameonyeshwa kuwa na uwezo wa kuboresha kumbukumbu na afya ya ubongo. Polyphenols katika matunda haya yana jukumu katika kuboresha afya ya ubongo na kuzuia uharibifu wa seli za ubongo.

  9. 🍇 Matunda ya mzabibu ni chanzo kizuri cha nishati. Kwa sababu ya sukari asili iliyomo, matunda haya yanaweza kutoa nguvu na kuongeza kiwango chako cha nishati katika siku yako.

  10. 🍇 Kwa wale wanaopenda kupunguza uzito, matunda ya mzabibu yanaweza kuwa msaada mzuri. Kwa kuwa yana kiwango cha chini cha kalori na mafuta, yanaweza kusaidia katika kudhibiti hamu ya kula na kusaidia katika kupunguza uzito.

  11. 🍇 Kumbuka, ingawa matunda ya mzabibu ni yenye manufaa kwa afya, ni muhimu kula kwa kiasi. Kula matunda mengi sana ya mzabibu kunaweza kuwa na athari hasi kama vile kuongeza uzito na kuathiri viwango vya sukari mwilini.

  12. 🍇 Kwa upande mwingine, unaweza pia kufurahia faida za matunda ya mzabibu kupitia juisi yake. Juisi ya mzabibu inaweza kuwa chaguo nzuri kwa wale ambao hawapendi kula matunda yenyewe.

  13. 🍇 Je, umewahi kufikiria kutumia matunda ya mzabibu kwenye sahani yako ya salad? Matunda haya yanaweza kuongeza ladha na ladha ya kipekee kwenye saladi yako na pia kuongeza faida ya kiafya.

  14. 🍇 Unaweza pia kuongeza matunda ya mzabibu kwenye smoothie yako ya asubuhi. Itakupa ladha tamu na virutubisho muhimu kwa mwili wako.

  15. 🍇 Kwa kuhitimisha, matunda ya mzabibu ni chakula kizuri sana kwa afya yetu na inaweza kuongeza ladha katika milo yetu ya kila siku. Kama AckySHINE, napendekeza kujumuisha matunda haya matamu katika lishe yako na kufurahia faida zake nyingi!

Je, umewahi kula matunda ya mzabibu? Una maoni gani kuhusu faida zake? Tuambie katika sehemu ya maoni hapa chini! 🍇😊

Mapishi ya samaki aina ya salmon

Wakati mwingine mtu unakuwa umechoka na usingependa kupoteza muda jikoni, so mlo wa chapchap unakuwa ni wazo zuri, Mlo huu ni rahisi kuuanda na hata haikuchukui zaidi ya dakika ishirini chakula kinakuwa tayari mezani.

Mahitaji

Salmon fillet 2
Potatao wedge kiasi
Lettice kiasi
Cherry tomato
Limao 1
Swaum
Chumvi
Olive oil

Matayarisho

Mmarinate samaki na chumvi, swaum na nusu ya limao kisha muweke pembeni, baada ya hapo washa oven kisha tia potato wedge zikisha karibia kuiva anza kumpika samaki, tia mafuta kidogo sana kama kijiko kimoja cha chai hivi katika frypan isiyoshika chini yakisha pata moto kiasi muweke samaki wako (upande wenye ngozi chini kwanza) Mpike mpaka uone rangi ya kahawia kwa chini kisha mgeuze upande wa pili, uku samaki wako akiwa anaendelea kuiva, tayarisha salad yako kwa kusafisha lettice na nyanya kisha zichanganye pamoja kisha tengeneza salad dressing pembeni , kamua limao kisha tia olive oil na chumvi kidogo, Baada ya hapo samaki na potato wedge vitakuwa vimeiva, andaa mlo wako na utakuwa tayari kwa kuliwa.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About