Dengue ni moja kati ya homa kali inayodhoofisha na kuambatana na maumivu makali. Kwa sasa hakuna kinga ya homa ya dengue, njia pekee ya kuepuka ugonjwa huu ni kuzuia kuumwa na mbu anayesambaza homa ya dengue.
Dalili za ugonjwa huu ni;
•Homa kali ya ghafla
•Maumivu makali ya kichwa
•Macho kuuma
•Maumivu ya viungo
•Kichefuchefu
•Kutapika
•Vipele ambavyo hutokea siku nne baada ya homa kuanza
•Kutoka damu puani, kwenye fizi na kuchubuka kirahisi
Mara nyingi dalili huwa sio kali na wengi hudhania ni homa ya mafua au maambikizi mengine ya virusi. Dalili hizi huanza kutokea baada ya wiki mbili, lakini kwa wengi huchukua wiki moja ya kwanza na tayari utaanza kuona dalili za dengue.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE