Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ya Ng'ombe Na Nyanya

Featured Image

Vipimo

Mchele (Basmati) - 3 vikombe

Nyama ya ngo’mbe - 1 kg

Pilipili boga - 1 kubwa

Nyanya - 2 kubwa

Vitunguu maji - 2 vikubwa

Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Tangawizi - 1 kijiko cha chai

Ndimu - 1

Mafuta ya kupikia - ½ kikombe

Mdalasini - ½ kijiko cha chai

Binzari nyembamba - 1 kijiko cha chai

Pilipili manga - ½ Kijiko cha chai

Hiliki - ½ Kijiko cha chai

Namna ya kutayarisha na Kupika

Roweka mchele wako katika chombo

Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi

Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi

Katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni

Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia

Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto

Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya

Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi

Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke

Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza

Funika na punguza moto na uache uive taratibu

Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Jinsi ya kutengeneza Pilau Ya Kuku

Mahitaji

Mchele wa basmati - 3 vikombe

Kuku - ½

Viazi - 4

Vitunguu - 2... Read More

Kupima lishe au afya ya mtu

Kupima lishe au afya ya mtu

Njia za kupima Afya

Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;

Read More
Mapishi Bora kwa Familia Yote Kupenda

Mapishi Bora kwa Familia Yote Kupenda

Mapishi Bora kwa Familia Yote Kupenda 🍽️

Karibu tena kwenye makala ya AckySHINE ambap... Read More

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Viambaupishi Vya Masala

Nyama vipande - 3 LB

Mtindi - ½ kopo

Kitunguu (thomu... Read More

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Wiki Nzima cha Lishe Bora 🥗

Hakuna jambo bora kuliko... Read More

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mahitaji

Kunde (Ila mimi nilitumia Nigerian brown beans 1/2 kilo)
Vitunguu maji (oni... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi

VIAMBAUPISHI

Unga - 3 Vikombe vya chai

Siagi - 250 gms

Baking powder - 3 Viji... Read More

Vitu 10 Rahisi na Salama vya Kuandaa kwa Chakula kimoja

Vitu 10 Rahisi na Salama vya Kuandaa kwa Chakula kimoja

Vitu 10 Rahisi na Salama vya Kuandaa kwa Chakula kimoja

Leo, kama AckySHINE, ningependa ku... Read More

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mahitaji

Ndizi mbichi 6
Nyama ya ng'ombe (nusu kilo)
Viazi mviringo 2
Kitu... Read More

Mapishi ya Chapati za Kusukuma kitaalamu

Mapishi ya Chapati za Kusukuma kitaalamu

Mahitaji

Unga wa ngano (plain flour 1/2 of kilo)
Siagi (butter vijiko 2 vya chakula)... Read More

Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)

Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)

Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi i... Read More

Utayarishaji bora wa chakula

Utayarishaji bora wa chakula

· Osha mikono yako kwa sabuni kabla na baada
ya kutayarisha chakula
· Tumia vyombo sa... Read More