Sidebar with Floating Button
Vichekesho vya AckySHINE
AckyShine

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Featured Image

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali ‘Salamu Malkia’ na kuongezea, ‘Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.

P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Lucy Kimotho (Guest) on September 20, 2017

🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo

Tabitha Okumu (Guest) on August 24, 2017

🙏💖💫 Mungu ni mwema

Isaac Kiptoo (Guest) on August 13, 2017

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Miriam Mchome (Guest) on July 16, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Rose Kiwanga (Guest) on June 30, 2017

🙏❤️ Mungu ni mwaminifu

James Mduma (Guest) on June 3, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Rose Kiwanga (Guest) on May 29, 2017

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Christopher Oloo (Guest) on April 30, 2017

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Anna Malela (Guest) on December 5, 2016

🙏✨ Mungu asikie maombi yetu

Lydia Mahiga (Guest) on November 14, 2016

🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku

Frank Macha (Guest) on September 8, 2016

🙏💖 Nakushukuru Mungu

Sarah Karani (Guest) on August 11, 2016

Rehema hushinda hukumu

Charles Mchome (Guest) on August 11, 2016

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Joyce Aoko (Guest) on July 11, 2016

🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie

Diana Mallya (Guest) on April 11, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Joseph Mallya (Guest) on December 4, 2015

🙏🙏🙏

Hellen Nduta (Guest) on November 5, 2015

Nakuombea 🙏

Peter Mbise (Guest) on October 23, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Peter Mbise (Guest) on September 23, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Esther Cheruiyot (Guest) on August 25, 2015

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Francis Mrope (Guest) on May 23, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Nancy Kawawa (Guest) on May 7, 2015

Dumu katika Bwana.

Esther Nyambura (Guest) on April 3, 2015

🙏🌟 Mbarikiwe sana

Related Posts

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Kwa jina la Baba….. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,M... Read More
Kuweka nia njema

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo n... Read More

SALA YA KUTUBU

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukiz... Read More

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

SALA YA UHAI KWA MT. YOSEFU

(Sala hii inafaa sana kwa ajili ya kutetea uhai wa watoto wachanga wakiwa tumboni mwa mama za... Read More

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More

Kanuni ya imani

Kanuni ya imani

Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi,/ mwumba mbingu na dunia./ Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)