Updated at: 2024-05-25 15:24:28 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
sura yako haifutiki usoni mwangu kirahic,ingawa upo mbal nami lkn penzi lako bado nalikumbuka,hakuna anayeweza kukata kiu yangu zaidi yako,nakupenda mpenzi wangu!
SMS nzuri ya mapenzi ya kimahaba ya kutuma kwa mpenzi wako umpendaye
Updated at: 2024-05-25 15:36:39 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu. Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka. Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika. Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka. Kitale katikati yake ukila utaridhika.
Updated at: 2024-05-25 15:37:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka. Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika. Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka. Kitale katikati yake ukila utaridhika. Matamu na maji yake hukata kiu haraka. Weupe watui lake lina ladha ukipika. Kupaka mafuta yake mwili hulainika. Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika. Hata na upepo wake uvumapo utacheka. Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema