Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS๐Ÿ’Œ๐Ÿ’•
โ˜ฐ
AckyShine

Jifunze kitu kupitia kisa hiki cha mume na mke

Featured Image

Mwanaume mmoja alimuoa mwanamke mrembo. Alikuwa akimpenda sana. Siku moja mwanamke alipatwa na maradhi ya ngozi. Kidogokidogo alianza kupoteza urembo wake.
.
.
.


Mume alipata safari na wakati akirudi alipata ajali iliyomfanya apoteze uwezo wake wa kuona. Hata hivyo, maisha yao ya ndoa yaliendelea kama kawaida. Lakini kadiri siku zilivyosonga mbele ndivyo mke alivyoendelea kupoteza urembo wake. Kwa kuwa mume alikuwa kipofu hakulijua hilo na hivyo hakuna kilichobadilika kwenye upendo wao. Aliendelea kumpenda, na mke alimpenda sana mumewe.
.
.
.


Siku moja mke alifariki dunia. Ilikuwa huzuni kubwa sana kwa mume.
Baada ya kumaliza taratibu zote za maziko, mazishi na kutandua msiba, alipanga kuhama kwenye mji huo na kwenda kuishi kwenye mji mwingine.
.
.
.


Mtu mmoja aliposikia habari hiyo alimwendea na kumuuliza: โ€œSasa utawezaje kutembea peke yako? Maana siku zote hizi mkeo alikuwa akikusaidia kukuonesha njia.โ€


Akajibu: โ€œMimi si kipofu. Nilifanya ionekane hivyo kwa sababu angejua kwamba ninauona mwili wake ulivyobadilika kuwa mbaya angepata maumivu makubwa zaidi kuliko ugonjwa wake wenyewe. Alikuwa mke mwema sana. Nilitaka aendelee kuwa na furaha.โ€
.
.
.


FUNZO:


Wakati fulani ni vizuri ukajifanya kipofu na kuyapuuza mapungufu ya mwenzako ili kumfanya awe mwenye furaha.


Meno huungโ€™ata ulimi mara nyingi, lakini vinaendelea kuishi pamoja kinywani. Huo ndio moyo wa KUSAMEHEANA. Macho hayaonani, lakini yanatazama na kuona vitu kwa pamoja, hupepesa na kulia pamoja. Huo unaitwa UMOJA.


1. Ukiwa peke yako unaweza kuongea, lakini ukiwa pamoja na mwenzako mnaweza KUZUNGUMZA.


2. Ukiwa peke yako unaweza KUFURAHI, lakini ukiwa na mwenzako unaweza KUFURAHIA.


3. Ukiwa peke yako unaweza KUTABASAMU, lakini ukiwa na mwenzako mnaweza KUCHEKA.


Huo ndio UZURI wa mahusiano yetu kama binadamu. Tunategemeana.


Kiwembe kina ukali lakini hakiwezi kukata mti; shoka lina nguvu na imara lakini haliwezi kukata nywele.


*Kila mtu ni muhimu kulingana na kusudio na lengo la uwepo wake. Usimdharau mtu yeyote kwa hali yoyote, kwa sababu huwezi kuwa yeye.


Mwenyezi Mungu atujaalie nguvu na moyo wa kusamehe, kustahmiliana na kuishi kwa umoja.
.
Tafakari
Mm na ww tunaweza kufanya haya!!!






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Vidokezo vya Kuepuka Mazungumzo ya Kuchosha na Msichana

Vidokezo vya Kuepuka Mazungumzo ya Kuchosha na Msichana

Mazungumzo ni sehemu muhimu katika uhusiano wowote wa kimapenzi. Lakini kuna wakati mazungumzo ya... Read More

Ushauri kwa vijana wenye miaka 22 nakuendelea

Ushauri kwa vijana wenye miaka 22 nakuendelea

Ikiwa wewe ni kijana na Una umri wa kuanzia miaka 22 na Kuendelea
Soma hapa ujifunze maisha ... Read More

Jinsi ya Kukuza Nguvu ya Uhusiano wa Ndugu katika Familia yako

Jinsi ya Kukuza Nguvu ya Uhusiano wa Ndugu katika Familia yako

Asante kwa kuchagua kusoma makala yetu kuhusu jinsi ya kukuza nguvu ya uhusiano wa ndugu katika f... Read More

Jinsi ya Kufanya Maamuzi ya Familia yanayofaa: Vidokezo na Mbinu Bora

Jinsi ya Kufanya Maamuzi ya Familia yanayofaa: Vidokezo na Mbinu Bora

Karibu katika mwongozo wetu wa jinsi ya kufanya maamuzi ya familia yanayofaa. Kama unavyojua, fam... Read More

Kuelewa na Kuheshimu Matakwa ya Kijinsia: Kuunda Mazingira Salama na Furaha

Kuelewa na Kuheshimu Matakwa ya Kijinsia: Kuunda Mazingira Salama na Furaha

  1. Kuelewa na kuheshimu matakwa ya kijinsia ni jambo muhimu katika kujenga mazingira salama na... Read More
Jinsi ya Kuwa na Muda wa Kufurahia: Kuweka Usawa kati ya Kazi na Familia

Jinsi ya Kuwa na Muda wa Kufurahia: Kuweka Usawa kati ya Kazi na Familia

Karibu kwenye mada yetu ya leo ambapo tutazungumzia jinsi ya kuwa na muda wa kufurahia kwa kuweka... Read More

Jinsi ya Kufurahia Wakati Pamoja: Kuweka Mawasiliano ya Karibu katika Familia yako

Jinsi ya Kufurahia Wakati Pamoja: Kuweka Mawasiliano ya Karibu katika Familia yako

  1. Anza kwa kujenga mawasiliano ya karibu na familia yako. Kila siku, tafuta muda wa kuzungumz... Read More
Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Uwazi katika Familia: Kuweka Nafasi ya Mazungumzo na Ufahamu

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Uwazi katika Familia: Kuweka Nafasi ya Mazungumzo na Ufahamu

  1. Familia ni sehemu muhimu sana katika maisha yetu na inaweza kuathiri sana maendeleo yet... Read More

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Kusisimua Mwili na Akili: Jinsi ya Kuleta Msisimko katika Kufanya Mapenzi

Mapenzi ni moja ... Read More

Jinsi ya Kudumisha Tamaduni na Desturi katika Familia yako

Jinsi ya Kudumisha Tamaduni na Desturi katika Familia yako

Kudumisha tamaduni na desturi katika familia yako ni muhimu sana kwa sababu inasaidia kuhifadhi u... Read More

Kuweka Kipaumbele cha Kuendeleza Maadili na Maadili ya Familia katika Nyumba Yako

Kuweka Kipaumbele cha Kuendeleza Maadili na Maadili ya Familia katika Nyumba Yako

Kuweka kipaumbele cha kuendeleza maadili na maadili ya familia ndani ya nyumba yako ni muhimu san... Read More

Jinsi ya Kujenga Ushirikiano wenye Msingi imara katika Mahusiano yako

Jinsi ya Kujenga Ushirikiano wenye Msingi imara katika Mahusiano yako

Karibu kwenye makala hii ambayo itakupa mbinu mbalimbali kuhusu jinsi ya kujenga ushirikiano weny... Read More