Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Mambo ya Msingi kuyajua Ili uishi na watu vizuri

Featured Image

Nimezipenda hizi nasaha. Naamini na nyinyi wenzangu hamtakosa japo machache ya kujifunza:-
1. Epuka hasira za ovyo na kila mtu, kuwa msikivu kabla ya kukimbilia maamuzi (elewa kuwa ukiwa na hasira huwezi kupata suluhu ya jambo)
2. Usiwatendee wengine ubaya ukadhani kuwa utakuwa salama (ubaya hulipwa kwa ubaya, ipo siku ubaya wako kwa wengine utakurejea kama sio kuwarejea watu wa kizazi chako)


3. Usichukue maamuzi kabla ya kutafiti ukweli (pengine wapo wanadamu wanaopenda kuonekana wao wema kwa kuumiza wengine). Mtuhumu mtu lakini mpe muda wa kumsikiliza, usimshambulie mtu kwa maneno makali bila kuujua ukweli, ukijua ukweli nafsi inaweza kukusuta.


4. Mchukulie kila mwanadamu ni mkosaji (tambua kuwa hata wewe unawakosea sana wengine na wanakuvumilia. Hivyo usiwe mwepesi wa kuwaadhibu wenzio kwa ubaya).


5. Usipande mbegu ya chuki na ubaya katika jamii unayoishi ukadhani itakuacha salama (chuki hukua kama mti utambaao, ukiipanda ndani ya jamii yako, haitatoka kwako na inaweza kutafuna kizazi chako ukajutia.


6. Tambua kuwa yule unayeishi nae ni mwanadamu kama wewe, mpe heshima na mwonyeshee upendo hata kama huoni anafanana nawe. Maisha ni duara huenda ulikuwa kama yeye au atakuja kuwa kama wewe baadae.


6. Usiwe muongeaji ovyo ovyo na usiye na subira. Kuongea sana kunapoteza busara.


7. Jiepushe na maisha ya kusukumwa na wengine kufanya jambo usilojua manufaa yake. Jifunze kujitegemea kiakili. Sio kila unayemdhania rafiki moyoni mwake yupo pamoja nawe, na ukashirikiana nae, wengi wa marafiki zetu hututumia sana kuliko tunavyoweza kuwatumia wao.


8. Usipende sana kugombana na watu kwa njia ya maongezi yanayodumu kama vile, ujumbe wa maandishi, mawasiliano ya simu au ujumbe wa maneno (SMS). Kumbuka kuwa maneno yanaishi kuliko ugomvi au uadui, ipo siku yatakurudi na utajiona mpumbavu na kukosa pa kujificha. Jifunze kusubiri.


9.Usifumbue mdomo wako kutamka ubaya au kunyanyua kidole chako kuandika ubaya juu ya mwenzio bila kujiuliza mara mbili moyoni mwako hatima ya unachokitoa kwa mwingine.


10. Jishushe na jifunze kusikiliza wengine wakati wa mazungumzo ili uweze kujifunza kabla ya kukurupuka kujibu, usikivu ni kipimo cha busara, mtu anayekurupuka kujibu jibu kila anachosikia hawezi kuwa kiongozi, Mume au Mke mwema kwani mara nyingi atapotoka tu.


10. Usitunze hasira nyingi moyoni kwani hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu. Jitahidi pia kuepuka kuwa na hasira mara kwa mara na zisizo na maana. Elewa kuwa hasira zisizo maana hukupunguzia maisha na kukupa maumivu wewe mwenyewe kuliko yule uliyemfanyia hasira, utakufa kwa magonjwa kabla ya wakati ufaao.


11. Thamani yako inategenezwa na watu wengine, wewe kama ni mtoto, mheshimu sana mzazi wako na kama umeoa au kuolewa, heshimu wazazi na familia ya mke au mumeo kwa kuwa bila wao, usingekuwa hivyo ulivyo leo unajivunia ndoa njema, kwa kuwa yupo mtu alimzaa huyo mwenzio. Mheshimu kwa lolote liwe jema au baya, utalipwa kwa wakati ufaao.


13. Usijibizane na mtu usiyemjua au ambaye hawezi kukupunguzia kitu katika maisha yako. Tambua kuwa unapunguza sehemu kubwa ya maisha yako kwa kutafuta magomvi na mtu wa mbali nawe.


14. Kumbuka asili yako, kumbuka upo hapo kwa kuwa kuna mahali ulitoka, maisha yanabadilika, usidharau pale ulipokuwa zamani kwa kuwa ndipo palipokufanya leo uwe hapo.


15. Subiri, sikiliza, elekeza, vumilia. Elewa sio kila mtu ana uelewa kama wako. Jitahidi kuwa mvumilivu katika kila jambo, usiinuke kuwafokea au kuwakaripia wengine kwa jambo ambalo pengine nao wanahitaji muda kueleweshwa ili walifanye vyema. Kumbuka sana, kuna wakati nawe ulikuwa huelewi kabisa lakini wapo wenzio walikuvumilia, wakakuelekeza njia njema, kufokea wengine mara kwa mara sio njia njema ya kuwafundisha bali ni kuwaweka mbali nawe.


Kumbuka: Ishi kwa kumpendeza Mungu.






Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE




Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke





Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.





[products columns="2" ids="30827"]


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuendelea Kujifunza na Kukua katika Ndoa

Jinsi ya Kuendelea Kujifunza na Kukua katika Ndoa

Kuendelea kujifunza na kukua katika ndoa ni muhimu sana kwa ustawi wa uhusiano wenu na kujenga ndoa ... Read More
Jinsi ya Kusaidia Watoto kukabiliana na Changamoto: Kuwa Msaada katika Kila Hatua

Jinsi ya Kusaidia Watoto kukabiliana na Changamoto: Kuwa Msaada katika Kila Hatua

Karibu kwenye makala hii ambayo itakupa maelezo juu ya jinsi ya kusaidia watoto kukabiliana na ch... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha usawa na haki za watoto wenu

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha usawa na haki za watoto wenu

Leo nitazungumzia juu ya jinsi wewe na mpenzi wako mnaweza kusaidiana katika kujenga na kudumisha... Read More

Jinsi ya Kuanzisha Mawasiliano ya Kwanza na Msichana

Jinsi ya Kuanzisha Mawasiliano ya Kwanza na Msichana

Leo, tutazungumzia jinsi ya kuanzisha mawasiliano ya kwanza na msichana. Ni muhimu sana kwa kila ... Read More

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya asubuhi au jioni?

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya asubuhi au jioni?

Habari wapenzi wa blogu yetu! Leo, tutazungumzia suala la ngono na wakati bora wa kufanya mapenzi... Read More

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aonekuwa Muhimu katika Maisha Yako

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aonekuwa Muhimu katika Maisha Yako

Mwanamke ni hazina kubwa katika maisha ya kila mwanaume. Ni kiumbe chenye thamani, cha thabiti na... Read More

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Ushirikiano katika Familia: Kuhamasisha Ushirikiano wa Timu

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Ushirikiano katika Familia: Kuhamasisha Ushirikiano wa Timu

  1. Shughulikia masuala yako ya kibinafsi kabla ya kujihusisha na familia yako. Unapojihusi... Read More

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya usalama na ulinzi wa familia yenu

Jinsi ya Kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala ya usalama na ulinzi wa familia yenu

Habari za leo wapendwa! Leo tutaongea kuhusu jinsi ya kuwasiliana na mpenzi wako kuhusu masuala y... Read More

Jinsi ya Kuanza Mazungumzo na Msichana Unayempenda

Jinsi ya Kuanza Mazungumzo na Msichana Unayempenda

Kuanza mazungumzo na msichana unayempenda inaweza kuwa vigumu, lakini pia inaweza kuwa jambo la k... Read More

Jinsi ya Kusimamia tofauti za maoni na migogoro katika uhusiano wa mapenzi

Jinsi ya Kusimamia tofauti za maoni na migogoro katika uhusiano wa mapenzi

Kusimamia tofauti za maoni na migogoro ni sehemu muhimu ya kujenga uhusiano wa mapenzi wenye afya. H... Read More
Jinsi ya Kukuza Nguvu ya Uhusiano wa Ndugu katika Familia yako

Jinsi ya Kukuza Nguvu ya Uhusiano wa Ndugu katika Familia yako

Asante kwa kuchagua kusoma makala yetu kuhusu jinsi ya kukuza nguvu ya uhusiano wa ndugu katika f... Read More

Kuimarisha Mazungumzo ya Uaminifu na Heshima katika Mahusiano

Kuimarisha Mazungumzo ya Uaminifu na Heshima katika Mahusiano

Mahusiano yoyote yana uzoefu wa changamoto, lakini kuwa na mazungumzo ya uaminifu na heshima ndiy... Read More