Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Kuna aina ngapi za dawa za kulevya?

Featured Image

Tunatofautisha dawa za kulevya katika makundi mawili. Zile zinazokubalika na zile zisizokubalika kisheria. Tanzania, dawa za kulevya zinazokubalika kisheria ni pamoja na tumbaku na pombe, pia dawa zilizothibitishwa kwa maandishi na daktari. Dawa zinazotolewa kwa udhibitisho wa madaktari ni zile dawa za kutibu. Pale zinapotolewa kwa sababu nyingine mbali na matibabu au maelezo ya daktari zinakuwa dawa za kulevya. Miongoni mwa dawa zinazotumika vibaya hapa Tanzania ni valium, asprin na panado. Vimiminika kama petroli pia hutumiwa kama dawa za kulevya. Vitu hivi hutumiwa kwa njia ya kuvuta hewa yake kwa pua au mdomo.
Pia kuna vileo visivyoruhusiwa ambavyo hutengenezwa kienyeji kama vile gongo. Dawa za kulevya ambazo hutumika sana Tanzania ni pamoja na bangi, mirungi, mandrax, heroini na kokaini. Kokaini ambayo hupatikana katika hali ya ungaunga ulio mweupe, hutumiwa kwa njia ya kuvuta kwa pua au kuchanganywa na maji na baadaye kujidunga mwilini kwa kutumia sindano. Heroini pia hupatikana kama unga mweupe. Unaweza kuvuta heroini kama sigara au kuvuta hewa yake kwa ndani na pia kwa kujidunga sindano. Katika hali i i isiyo ya kawaida heroini vilevile inaweza kupatikana katika vipande vidogovidogo vya kahawia vijulikanavyo kama β€œsukari ya kahawia”.
Njia nyingine ya kuzungumzia dawa za kulevya ni kutokana na madhara yake. Yapo madawa ambayo hupagawisha au yanayozubaisha au kupoozesha kama vile kileo, nikotini, dawa za usingizi, kwa mfano valium na heroini. Dawa hizo zinamfanya mtumiaji kujisikia shwari, lakini pia huhuzunisha. Dawa zinazochamngamsha ni i kama mirungi, kokaini na zile za kuvuta, kwa mfano petroli, zina madhara ya kukufanya uhamasike na kujisikia kuwa na nguvu. Dawa zinazopagawisha zinaleta hisia, sauti, taswira, harufu kwa mtu japokuwa vyote hivyo havipo kweli. Bangi ni mojawapo ya dawa hizi.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Kujikinga na Mimba

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wangu kuhusu Kujikinga na Mimba

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wako kuhusu Kujikinga na Mimba

Karibu sana marafiki zangu! L... Read More

Uhusiano wa ubakaji na uvaaji wa nguo fupi?

Uhusiano wa ubakaji na uvaaji wa nguo fupi?

Ubakaji kamwe siyo kosa linalomhusu yeye aliyebakwa; ni kosa
linalomuhusu yeye aliyebaka. Un... Read More

Je, ni lazima kumeza vidonge vya kuzuia mimba siku zote, hata zile siku nisipojamiiana?

Je, ni lazima kumeza vidonge vya kuzuia mimba siku zote, hata zile siku nisipojamiiana?

Ndiyo, vidonge vya kuzuia mimba ni lazima vimezwe kila siku hata kama hufanyi ngono siku hiyo. Ku... Read More

Je, ni sahihi kutumia michezo ya ngono/kufanya mapenzi kama sehemu ya uhusiano?

Je, ni sahihi kutumia michezo ya ngono/kufanya mapenzi kama sehemu ya uhusiano?

Je, ni sahihi kutumia michezo ya ngono/kufanya mapenzi kama sehemu ya uhusiano? Hili ni swali amb... Read More

Jinsi ya Kuwa na Siku ya Kumbukumbu ya Kipekee na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Siku ya Kumbukumbu ya Kipekee na Msichana

Kumbukumbu zetu ni muhimu sana katika maisha yetu. Siku ya kumbukumbu ni siku muhimu sana kwa sab... Read More

Vidokezo vya Kuwa na Uhusiano Wenye Furaha na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Uhusiano Wenye Furaha na Msichana

Kuwa na uhusiano wenye furaha na msichana ni jambo ambalo kila mwanaume anatamani. Lakini mara ny... Read More

Kuna fikra kuwa Albino ni watu wa kawaida je, kisayansi hii ni kweli?

Kuna fikra kuwa Albino ni watu wa kawaida je, kisayansi hii ni kweli?

Hii ni kweli kabisa. Watu wanaoishi na ualbino ni watu wa
kawaida kama binadamu wengine wote... Read More

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono?

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono?

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono? 😊

  1. Kwanz... Read More

Kwa nini sio Sahihi Kufanya Ngono na Mtu Mmoja wa Marafiki?

Kwa nini sio Sahihi Kufanya Ngono na Mtu Mmoja wa Marafiki?

Kwa nini sio Sahihi Kufanya Ngono na Mtu Mmoja wa Marafiki? πŸŒΈπŸ’”

Jambo zuri siku zote ... Read More

Iwapo mtu mzima amejamiiana na mtoto na wote wawili wamekubaliana

Iwapo mtu mzima amejamiiana na mtoto na wote wawili wamekubaliana

Ni kweli hiyo ni dhuluma na inaitwa unyanyasaji wa kijinsia kwa
mtoto. Watoto wanaweza kusha... Read More

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi yenye michezo ya kubahatisha?

Je, watu wanapendelea ngono/kufanya mapenzi ya kawaida au ngono/kufanya mapenzi yenye michezo ya kubahatisha?

Je, unajua kwamba wengi wetu tunapenda kufanya mapenzi ya kawaida? Na pia unajua kwamba kuna wale... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili mawazo na hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kujadili mawazo na hisia wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Kwa wengi, ngono inaonekana kama kitendo cha kimwili tu bila ya umuhimu wa kujadili mawazo na his... Read More