Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Madhara ya dawa za kulevya kwa mwili na ubongo

Featured Image
Moja kati ya vitu vinavyotisha kuhusu dawa za kulevya ni kwamba zinaathiri watu kwa njia mbalimbali na huwezi ukasema kwa uhakika jinsi zitakavyokuathiri. Madhara ya dawa za kulevya yanategemea aina, kiwango na jinsi zitakavyotumika. Vilevile inategemea na umri, afya ya mwili na ukomavu wa akili, na pia mazoea ya matumizi ya dawa hizo.
Madhara ya muda hutokea mara tu baada ya dawa za kulevya kutumika, wakati madhara ya muda mrefu huonekana baada ya muda kupita, na mara nyingi husababisha uharibifu wa kudumu kwenye mapafu na ubongo.

Kwa mfano, bangi, husababisha kuongezeka kwa mapigo ya moyo, matatizo ya kumbukumbu ya muda mfupi, pamoja na umakini, kujifunza, kufikiri na kutatua matatizo. Pia inaweza ikasababisha kasoro kwenye utaratibu wa viungo vya mwili. Mara kwa mara wavuta bangi huwa na macho mekundu. Na vijana wengine hupata mihemuko mbalimbali kama uoga na hofu baada ya matumizi ya bangi.
Dawa za kulevya za vichangamsho, kama mirungi na kokaini, inasemekana kuwa huwafanya watumiaji kuwa macho, kujiona wana nguvu na kujiamini. Vichangamsho vikitumika kwa wingi, humfanya mtumaji kujihisi kuwa na wasiwasi au hofu. Matumizi mabaya ya dawa za kulevya kwa muda mrefu huweza kusababisha matatizo ya akili au hata kifo i iwapo yatatumika kwa kiwango cha juu.
Dawa za kulevya zinazokufanya upooze kama heroini au dawa nyingine zinazoagizwa na daktari, husababisha kujisikia umetulia, una amani na furaha. Ukizidisha vipimo husababisha usingizi, upungufu wa umakini na uwezo wa kuona, kizunguzungu, kutapika na kutokwa jasho. Vilevile kipimo kingi kinaweza kusababisha usingizi wa muda mrefu, kuzimia na hata kifo.

Pombe za kienyeji kama gongo ni hatari kwa afya na zinaweza kusababisha upofu na hata kifo.
Matumizi ya dawa za kulevya hupunguza uwezo wa vijana kuhimili na kutatua matatizo yao ya kijamii na kiakili. Hii husababisha vijana kuwa wepesi kujihusisha na ujambazi na mambo ya ngono na ugomvi, mabadiliko hayo ya tabia husababisha ugomvi katika familia na kuvunjika kwa urafiki. Matumizi ya dawa za kulevya ndiyo sababu kubwa ya ajali za barabarani, kujiua na maambukizo mbalimbali.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, mimi ni msichana Albino ninaweza kupata mimba kama nikijamiiana mara moja tu?

Je, mimi ni msichana Albino ninaweza kupata mimba kama nikijamiiana mara moja tu?

Ndiyo msichana anaweza kupata mimba kwa kujamiiana mara
moja tu bila kujali ana rangi gani y... Read More

Jinsi ya Kujilinda na Mimba Bila Kusababisha Madhara ya Kiafya?

Jinsi ya Kujilinda na Mimba Bila Kusababisha Madhara ya Kiafya?

Jinsi ya Kujilinda na Mimba Bila Kusababisha Madhara ya Kiafya? 😊🌼

Karibu kijana! Le... Read More

Je, watu wanaamini katika kutumia dawa za kuongeza hamu ya ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanaamini katika kutumia dawa za kuongeza hamu ya ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanaamini katika kutumia dawa za kuongeza hamu ya ngono/kufanya mapenzi? Hili ni swali a... Read More

Nini maana ya neno Albino?

Nini maana ya neno Albino?

Neno Albino linamaanisha mtu mweupe, linatokana na neno la lugha ya Kilatini - albus-linamaanisha β€... Read More
Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Simu na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mazuri ya Simu na Msichana

Kama una nia ya kuimarisha uhusiano wako na msichana, ni muhimu kuwa na mawasiliano mazuri ya sim... Read More

Vidokezo vya Kufanya Msichana Ahisi Anapendwa na Kuthaminiwa

Vidokezo vya Kufanya Msichana Ahisi Anapendwa na Kuthaminiwa

Habari za asubuhi wapendwa! Leo, tutajadili vidokezo muhimu ambavyo vitamsaidia msichana ahisi an... Read More

Kwa nini mara nyingi mvulana ni mwepesi sana katika kuanzisha kufanya mapenzi? Na kwa nini mwanaume mara nyingi anafikia mshindo kabla ya mwanamke? Mwanaume anawahi kufika kileleni kwa nini?

Kwa nini mara nyingi mvulana ni mwepesi sana katika kuanzisha kufanya mapenzi? Na kwa nini mwanaume mara nyingi anafikia mshindo kabla ya mwanamke? Mwanaume anawahi kufika kileleni kwa nini?

Kwa kawaida i inakubalika kuwa wavulana ndiyo waaanze kuonyesha ishara za kujamiaana na tafiti zi... Read More

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Ujasiri wa Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Ujasiri wa Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kukabiliana na Hisia za Kukosa Ujasiri wa Kujihusisha na Ngono? 🌈

Karibu kija... Read More

Je, kuna vitu fulani ambavyo hupendezwa nayo katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna vitu fulani ambavyo hupendezwa nayo katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna vitu fulani ambavyo hupendezwa nayo katika ngono/kufanya mapenzi? Ndio, kuna mambo mengi... Read More

Magonjwa yatokanayo na sigara

Magonjwa yatokanayo na sigara

Kuna matatizo na magonjwa mengi na ya aina mbalimbali
unayoweza kuyapata kutokana na utuvaji... Read More

Sababu za ukeketaji

Sababu za ukeketaji

Hakuna hata mmoja anayejua hasa kwa nini, na lini desturi
imeanza. Jamii inatoa maelezo tofa... Read More

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanasema kuwa unaweza kupona UKIMWI kwa kujamiiana na Albino. Hii ni kweli?

Watu wanaweza kuvumisha uongo wowote ili kupotosha
ukweli na kufanya mambo yao maovu wanayoy... Read More