Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS๐Ÿ’Œ๐Ÿ’•
โ˜ฐ
AckyShine

Dalili, athari, kinga na tiba ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)

Featured Image
Kifua kikuu ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vya bacteria na kuenezwa kwa njia ya hewa. Mtu mwenye maambukizi ya kifua kifua kikuu akikohoa, kupiga chafya au kutema mate ovyo husambaza vijidudu hewa, huweza kumwabukiza mtu mwingine kama atakuwa hajaanza kutumia dozi ya kifua kikuu.

Dalili za kifua kikuu.



  1. Kukohoa kwa muda wa wiki mbili au zaidi

  2. Maumivu ya kifua

  3. Homa za usiku

  4. Kutoka jasho kwa wingi usiku

  5. Kupungua uzito

  6. Kukohoa damu

  7. Kukosa hamu ya chakula na mwili kuwa dhaifu


Athari za kifua kikuu.



  1. Ugonjwa huweza kuenea kwenye viungo vingine vya mwili.

  2. Watu wengine hupoteza maisha iwapo hawatapata tiba sahihi mapema.

  3. Watu wengine huambukizwa ugonjwa katika muda mfupi.

  4. Wagonjwa wa kifua kikuu hawazezi kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendelea.

  5. Matibabu ya kifua kikuu huchua muda mrefu na ni gharama kubwa.


Kinga za ugonjwa wa kifua kikuu.


Ugonjwa huu unakingwa kwa chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu (BCG) ambayo hutolewa mara tu mtoto anapozaliwa.
Ili kupunguza uwezekano wa kupata kifua kikuu zingatia yafuatayo;


  1. Kujenga na kuishi kwenye nyumba zinazoruhusu mzunguko kwa hewa ya kutosha (ziwe na madirisha makubwa ya kutosha)

  2. Epuka kukaa kwenye msongamano wa watu wengi

  3. Watoto wanyonyeshwe maziwa ya mama pekee kwa miezi sita na umlikiza kwa vyakula vyenye virutubisho ili kumjengea kinga imara

  4. Kula vyakula vyenye lishe bora

  5. Kutotema mate na makohozi ovyo ili kuziua usambaaji wa bacteria wasababishao Kifua kikuu.


Ratiba ya chanjo.


Chanjo ya kifua kikuu hutolewa baada ya mtoto kuzaliwa au anapofika kliniki kwa mara ya kwanza
Iwapo kovu kwa mtoto halijajitokeza chanjo irudiwe katika kipindi cha miezi 3.

Tiba ya kifua kikuu (TB)


Ugonjwa wa kifua kikuu unatibika. Matibabu yake huchukua muda mrefu wa miezi 6 hadi 8 na ni ya gharama kubwa.

Inashauriwa mgonjwa awahi matibabu mapema kwenye vituo vya kutolewa huduma za kinga.

Ugonjwa wa kifua kikuu ni hatari, hata hivyo unakingwa kwa chanjo.

Mzazi au mlezi hakikisha kila mtoto anapozaliwa anapata chanjo ya kuzuia kifua kuu

โ€œKumbuka chanjo ya kifua kikuu (BCG) Itamkinga mtoto dhidi ya ugonjwa wa kifua kikuuโ€.
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kuongeza wingi wa mbegu za kiume

Jinsi ya kuongeza wingi wa mbegu za kiume

Ili kuongeza mbegu za kiume zingatia haya yafuatayo;

Kula lishe bora

Chakula unacho... Read More

Matumizi ya zabibu kavu kutibu shinikizo la chini la damu

Matumizi ya zabibu kavu kutibu shinikizo la chini la damu

Zabibu huweza kutumika kama tiba ya shinikizo la chini la damu kama ifuatavyo

1. Chukua za... Read More

Faida za Korosho Kiafya

Faida za Korosho Kiafya

Korosho zina faida hizi zifuatazo;

1. Zinakinga Maradhi ya Saratani Haswa kwenye matumbo ma... Read More

Matumizi ya juisi ya limao kutibu shinikizo la chini la damu

Matumizi ya juisi ya limao kutibu shinikizo la chini la damu

Juisi hii ni nzuri sana katika kutibu shinikizo la juu la damu.

Lakini inaweza pia kutumika... Read More

Vyakula vinavyowezesha ubongo ufanye kazi kwa ufanisi

Vyakula vinavyowezesha ubongo ufanye kazi kwa ufanisi

  • Mafuta ya zeituni
  • Mafuta ya nazi
  • Samaki
  • Binzari
  • Mayai
  • Read More
Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya Dengu (Dengue fever)

Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya Dengu (Dengue fever)

Ugonjwa wa dengue ni tishio la ugonjwa hatari linaongezeka siku hadi siku. Dengue ni ugonjwa unao... Read More

Mambo ya Muhimu kuyajua kuhusu maumivu ya Korodani

Mambo ya Muhimu kuyajua kuhusu maumivu ya Korodani

Kuna wakati mwanaume huweza kupata maumivu ya korodani, ambapo inawezekana ikawa ni maumivu kwa k... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia aloe vera

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia aloe vera

Mshubiri au Aloe Vera kama ilivyozoeleka na namna nzuri kwa wale wote wanaotaka kubaki na ngozi ... Read More

Faida za kiafya za Kula Matunda

Faida za kiafya za Kula Matunda

Matunda yote yana faida mwilini kiafya lakini matunda yanatofautiana kifaida. Zifuatazo ni faida ... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia Mtindi na asali

Jinsi ya kutibu chunusi kwa kutumia Mtindi na asali

Kutumia mtindi na asali ni moja ya dawa rahisi zaidi za kutibu chunusi.

Unahitaji:

... Read More

Chanzo, dalili, aina na matibabu ya ugonjwa wa kifafa

Chanzo, dalili, aina na matibabu ya ugonjwa wa kifafa

Huu ni ugonjwa ambao unasabababishwa na seli zilizopo katika mishipa ya fahamu zilizopo kwenye ubong... Read More
Ushauri kuhusu mwili wako

Ushauri kuhusu mwili wako

Nimekutana na hiki kitabu japo nimekipitia juu juu nikaona nisiwe mchoyo Wa kukushirikisha wewe u... Read More