Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Nazi Wa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia, Mboga Ya Matembele Na Samaki Wa Kukaanga

Featured Image

Vipimo Vya Ugali

Unga wa mahindi - 4

Maji - 6 kiasi kutegemea na aina ya unga

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Weka maji katika moto.

Tia unga kidogo katika kibakuli, koroga ufanye uji.

Maji yakichemka tia kwenye maji uwe uji.

Ujii ikiiva punguza kidogo tia unga kidogokidogo na usonge ugali. Ikiwa unga ni mgumu utaongeza maji ya ule uji ulopunguza usonge hadi uive ukiwa tayari.

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nazi Kwa Nyanya Chungu/Mshumaa/Ngogwe Na Bamia

Nyanya chungu/mshumaa/Ngogwe - 7

Bamia - 10

Kitunguu maji - 2

Nyanya/tungule - 2

Tui la nazi jepesi - 2 viwili

Tui la nazi zito - 2

Chumvi - kiasi

Ndimu - 2 mbili kamua

Bizari manjano/haldi/turmeric - Β½ kijiko cha chai

Pilipili mbuzi - 3

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Katakata kitunguu maji na nyanya vipande vidogodogo sana kisha weka katika sufuria.

Iache ichemke kwa maji yake ya nyanya, ikishachemka tia maji kidogo kama robo kikombe.

Tia nyanya chungu, bamia na koleza ndimu, chumvi.

Iache ichemke. Inapokuwa tayari imeiva tia tui jepesi endelea kuacha katika moto huku unakoroga kidogo kidogo.

Tui jepesi likipungua kiasi chake, tia tui zito, kisha usiachie mkono koroga ikichemka kidog kiasi cha kuiva tui mchuzi tayari.

Vipimo Vya Mboga Ya Matembele

Matembele - 5 mafungu

Mafuta - ΒΌ kikombe

Kitunguu maji kilokatwakatwa - 1

Nyanya/tungule - 4

Chumvi - 1

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Punguza miche ya matembele kwa kuikata ncha kisha osha majani yake. Acha yachuje maji .
Weka mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji na nyanya hadi viivie.
Tia mboga, Iache ichemke kwa maji yake hadi iive. Ukiona bado haikuiva tia maji kidogo tu.
Ukipenda unatia ndimu kiasi cha kipande kimoja ukamue .

Samaki Wa Nguru Wa Kukaanga

Samaki Wa Nguru - 4 vipande

Kitunguu saumu(thom/galic) na tangawizi ilosagwa - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi - 4

Ndimu - 2 kamua

Bizari ya samaki - 1 kijiko cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki.
Mwache akolee viungo kwa muda kidogo.
Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Pasta za cream na uyoga

Mapishi ya Pasta za cream na uyoga

Mahitaji

Pasta (2 na 1/2 vikombe vya chai)
Uyoga (mashroom 2 vikombe vya chai)
... Read More

Mapishi ya Chicken Satay

Mapishi ya Chicken Satay

Mahitaji

Kidali cha kuku 1 (chicken breast)
Kitunguu maji 1/2 (onion)
Kitunguu ... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende Na Ufuta

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende Na Ufuta

MAHITAJI

Unga - 3 Vikombe vya chai

Baking powder - 1 Β½ Vijiko vya chai

Sukar... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tangawizi

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tangawizi

MAHITAJI

Unga - 2 Vikombe

Cocoa ya unga - 1 Kijiko cha supu

Sukari ya hudhuru... Read More

Jinsi ya kutengeneza Labania Za Maziwa

Jinsi ya kutengeneza Labania Za Maziwa

MAHITAJI

Maziwa ya unga - 2 vikombe

Sukari - 3 vikombe

Maji - 3 vikombe

Read More
Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Mara nyingi biringanya hutumika kama kiungo cha nyongeza katika mchuzi. Hata hivyo, kiungo hiki k... Read More

Mapishi ya Chapati za maji za vitunguu

Mapishi ya Chapati za maji za vitunguu

Mahitaji

Unga wa ngano (plain flour) 1/4
Kitunguu kikubwa (chopped/slice onion) 1Read More

Mapishi ya Mitai

Mapishi ya Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano - magi 2 (vikombe vikubwa)

Hamira kijiko 1 cha chai

<... Read More
Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Mapishi ya Wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Samaki Na Rojo La Bilingani Na Viazi/Mbatata

Wali Wa Nazi

Mpunga - 4 vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - Kiasi

Read More
Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Vipimo vya Wali:

Mchele - 3 vikombe

*Maji ya kupikia - 5 vikombe

*Kidonge cha s... Read More

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mahitaji

Mchele
Kisamvu kilichotwangwa
Samaki
Mbaazi
Nyanya chunguRead More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Ufuta Na Jam

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Ufuta Na Jam

VIAMBAUPISHI

Unga vikombe 2

Sukari ya kusaga 1/4 Kikombe

Siagi 250 gms

... Read More