Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Kamba Wa Nazi, Kisamvu Na Kachumbari Ya Papa Mkavu

Featured Image

Vipimo - Ugali

Maji - 4 vikombe kiasi inategemea na unga wenyewe.

Unga wa sembe - 2 vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani iliyolowanishwa na maji kisha upete pete huku ukiugeuza geuza mpaka ukae shepu nzuri ya duara.Weka tayari kwa kuliwa.

Vipimo - Mchuzi wa kamba wa nazi

Kitunguu - 1

Nyanya - 2

Kamba waliomenywa - 1 Kilo

Pilipili mbichi iliyosagwa - Β½ kijiko cha chai

Kitunguu saumu na tangawizi ilivyosagwa - 1 kijiko cha supu

Nazi nzito iliyochujwa - 1 kikombe

Bizari ya mchuzi - Β½ kijiko cha chai

Chumvi - Kiasi

Ndimu - Nusu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Safisha na osha kamba vizuri kisha mtie katika sufuria. Katia kitunguu, nyanya, tia chumvi, pilipili mbichi ya kusaga, thomu na tangawizi, bizari ya mchuzi na ndimu. Tia maji kidogo kiasi acha ichemke.
Watakapoiva na karibu kukauka, mimina tui la nazi taratibu koroga kiasi
Punguza moto aacha ichemke kidogo ukiwa mchuzi tayari.

Vipimo - Kisamvu

Kisamvu - 2 vikombe

Kunde mbichi zilizochemshwa - 1 kikombe

Kitunguu - 1

Nazi nzito iliyochujwa - 1 vikombe

Chumvi - Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Weka kisamvu katika sufuria, katia kitunguu, tia chumvi, maji kidogo acha kichemke.
Huku ikichemka mimina kunde mbichi zilizochemshwa acha zipikikie kidogo mpaka kisamvu kikaribie kukauka na kunde kuiva.
Mimina nazi nzito punguza moto acha ichemke kidogo, mimina kwenye bakuli tayari kwa kuliwa.

Vipimo - Kachumbari Ya Papa

Papa mkavu (au nguru) - kipande

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Muoshe papa vizuri atoke mchanga kisha mchome kwenye jiko la mkaa au unaweza kumtia kwenye treya kisha kwenye oven kwa moto wa 350 kwa dakika 15 mpaka 20.
Akikauka mchambue chambue weka kando.
Tengeneza kachumbari, kwa kukata kitunguu, nyanya na pilipili mbichi, tia ndimu na chumvi.
Changanya na papa mkavu uliyemchambu ikiwa tayari.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga

Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga

Vipimo

Wali:

Mchele mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi... Read More

Mapishi ya Wali wakukaanga

Mapishi ya Wali wakukaanga

Mahitaji

Mchele (Basmati rice) 1 kilo
Vitunguu (chopped onion) 2 vikubwa
Garlic... Read More

Mapishi ya Borhowa

Mapishi ya Borhowa

Mahitaji

Daal (lentils) nyekundu au/na kijani - 1 Kikombe kikubwa

Bizari ya manjano... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Viambaupishi: Wali

Mchele 3 Magi

Mafuta 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu ... Read More

Jinsi ya kutengeneza Labania Za Maziwa

Jinsi ya kutengeneza Labania Za Maziwa

MAHITAJI

Maziwa ya unga - 2 vikombe

Sukari - 3 vikombe

Maji - 3 vikombe

Read More
Jinsi ya kupika Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

Jinsi ya kupika Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

VIPIMO:

Unga wa Visheti

Unga 4 Vikombe vya chai

Siagi 1 Kikombe cha chai

<... Read More
Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama

Mahitaji

Ndizi mbichi 6
Nyama ya ng'ombe (nusu kilo)
Viazi mviringo 2
Kitu... Read More

Mchemsho wa samaki na viazi

Mchemsho wa samaki na viazi

Mahitaji

Samaki mbichi (1)
Viazi mbatata (3)
Nyanya (1)
Kitunguu maji
Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Jinsi ya kupika Wali Wa Karoti Na Nyama

Viambaupishi: Wali

Mchele 3 Magi

Mafuta 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu ... Read More

Mapishi ya Ugali, dagaa (wabichi) na matembele

Mapishi ya Ugali, dagaa (wabichi) na matembele

Mahitaji

Dagaa wabichi (Fresh anchovies packet 1)
Unga wa ugali (corn meal flour 1/4... Read More

Mapishi ya chipsi na samaki wa kuchoma

Mapishi ya chipsi na samaki wa kuchoma

Mahitaji

Viazi ulaya (baking potato 5 vya wastani)
Parprika 1 kijiko cha chai
P... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende Na Ufuta

Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende Na Ufuta

Viambaupishi

Unga 3 Vikombe vya chai

Baking powder 1 Β½ Vijiko vya chai

Sukar... Read More