Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga

Featured Image

Biriani ni miongoni mwa vyakula ambavyo ni nadra sana kupikwa katika familia nyingi tofauti na vyakula vingine. Inawezekana ni kutokana na watu wengi kutoelewa namna ya kuoika chakula hiki kutokana na kuhitaji viungo vingi ambavyo huwapa usumbufu wapishi.
Kuna aina mbalimbali za upishi wa biriani ambapo mara nyingi hutofautiana kutokana na viungo vinavyotumika katika upishi.
Biriani la mbogamboga ni miongoni mwa aina hizo za upishi. Chakula hiki kinaweza kuliwa na kila mtu hususan wale wasiotumia nyama wala samaki.

Mahitaji:

½ kg mchele wa basmati
Kitunguu maji kikubwa 1
Nyanya 1 kubwa
Karoti 1 kubwa
Njegere robo kikombe
Kiazi ulaya 1 kikubwa
Tangawizi za kusaga kijiko 1
Kitunguu swaumu cha kusaga kijiko 1
Karafuu kijiko 1
Majani ya kotimili fungu 1
Maziwa ya mtingi ¼ kikombe
Chumvi na pilipili kiasi
Unga wa dhani kijiko 1 cha mezani
Juisi ya limao kijiko 1 cha mezani
Mafua ¼ lita

Maandalizi:

Chemsha mchele na kisha weka pembeni
Osha mbogamboga zote isipokuwa vitunguu na nyanya
Changanya mtindi na tangawizi pamoja na kitunguu swaumu viache vikae kwa muda wa saa moja
Chukua sufuria weka mafuta na kisha kaanga vitunguu maji, weka nyanya, chumvi, kotimili na limao halafu weka karafuu na kanga hadi vichanganyike vizuri
Miminia mchanganyiko wa mtindi na baadaye weka pilipili na baadaye weka unga wa dhania
Chukua mchele uliochemshwa changanya na mchanganyiko huo
Palia moto juu ya chakula chako na acha kwa muda wa dakika 30
Baada ya hapo chakula chako cha biriani kitakuwa tayari kwa kuliwa

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Kabichi

Mapishi ya Kabichi

Mahitaji

Kabichi 1/2 kilo
Nyanya ya kopo 1/2
Kitunguu 1
Curry powder 1/2 k... Read More

Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri

Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri

Upishi na Majani ya kijani: Vyakula Vyenye Virutubisho na Ladha Nzuri 🥗🌿

Hakuna shak... Read More

Mapishi ya samaki aina ya salmon

Mapishi ya samaki aina ya salmon

Wakati mwingine mtu unakuwa umechoka na usingependa kupoteza muda jikoni, so mlo wa chapchap unak... Read More

Jinsi ya kutengeneza Cookies Za Tende Na Tangawizi

Jinsi ya kutengeneza Cookies Za Tende Na Tangawizi

MAHITAJI

Unga vikombe vikombe 4

Baking soda 1 kijiko cha chai mfuto

Siagi 400... Read More

Mapishi ya Wali Wa Nazi Wa Adesi, Bamia Na Mchuzi Wa Kamba

Mapishi ya Wali Wa Nazi Wa Adesi, Bamia Na Mchuzi Wa Kamba

Mahitaji

Mchele - 2 vikombe

Adesi -1 ½ vikombe

Nazi ya unga - 1 Kikombe

<... Read More
Jinsi ya kupika Mishkaki ya kuku

Jinsi ya kupika Mishkaki ya kuku

Kidali cha kuku 1 kikubwa
Swaum,tangawizi 1 kijiko cha chai
Limao 1/2
Pilipili ya ... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Njugu/Matunda Makavu (Rock Cakes)

Jinsi ya kupika Biskuti Za Njugu/Matunda Makavu (Rock Cakes)

Viambaupishi

Unga 4 Vikombe

Sukari 10 Ounce

Siagi 10 Ounce

Mdalasini ya... Read More

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ng’ombe Na Mchicha

Wali Wa Mpunga

Mchele wa mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - ... Read More

Mapishi ya Pasta za cream na uyoga

Mapishi ya Pasta za cream na uyoga

Mahitaji

Pasta (2 na 1/2 vikombe vya chai)
Uyoga (mashroom 2 vikombe vya chai)
... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Chumvi

VIAMBAUPISHI

Unga - 3 Vikombe vya chai

Siagi - 250 gms

Baking powder - 3 Viji... Read More

Madhara ya kula yai bichi

Madhara ya kula yai bichi

Yai bichi linaweza kuwa na vijidudu viitwavyo kwa kitaalamu “SALMONELLA” vinavyoweza kusababi... Read More

Upishi wa Afya kwa Kompyuta: Milo Rahisi na yenye Ladha

Upishi wa Afya kwa Kompyuta: Milo Rahisi na yenye Ladha

Upishi wa Afya kwa Kompyuta: Milo Rahisi na yenye Ladha 🍲🖥️

Hivi leo, AckySHINE an... Read More