Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Featured Image

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Maria Bikira Milele, na mkubwa wa Familia Takatifu. Umechaguliwa na Mwakilishi wa Kristu kama Msimamizi wa kimbingu na mlinzi wa Kanisa alilolianzisha Kristu. Ndiyo maana ninakuomba kwa matumaini makuu usaidizi wako wenye nguvu kwa ajili ya Kanisa zima duniani.

Mlinde kwa namna ya pekee, kwa upendo wa kikweli wa ki-baba, Baba Mtakatifu na Maaskofu wote na Mapadre wenye ushirika na Kiti cha Petro. Uwe mlinzi wao wote wanaotumikia wokovu wa wanadamu kati ya majaribu na mahangaiko ya maisha haya, na utujalie kwamba watu wote wa dunia hii wamfuate Kristu na Kanisa alilolianzisha.


Mpendwa Mtakatifu Yosefu, ukubali majitoleo ya nafsi yangu ambayo sasa ninafanya. Ninajiweka wakfu kwako kwa ajili ya utumishi wako, ili daima wewe uwe baba yangu, mlinzi wangu, na kiongozi wangu katika njia ya wokovu. Unijalie usafi mkuu wa moyo na matamanio makuu ya maisha ya kiroho. Unijalie ili matendo yangu yote, kwa mfano wako, yawe kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mungu, pamoja na Moyo wa kimungu wa Yesu, moyo safi wa Maria, na moyo wako wa ki-baba. Uniombee, nami nishiriki kifo chako cha furaha na kitakatifu.
Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Dorothy Nkya (Guest) on August 17, 2017

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Mwanaidi (Guest) on July 17, 2017

πŸ™πŸ™πŸ™

Michael Mboya (Guest) on May 23, 2017

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Daniel Obura (Guest) on March 6, 2017

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Grace Mligo (Guest) on February 5, 2017

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Peter Tibaijuka (Guest) on December 5, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Moses Kipkemboi (Guest) on November 17, 2016

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

David Chacha (Guest) on October 5, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Mary Njeri (Guest) on July 16, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Mercy Atieno (Guest) on June 2, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Joseph Mallya (Guest) on April 26, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

John Lissu (Guest) on April 25, 2016

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Robert Okello (Guest) on April 17, 2016

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Mariam Kawawa (Guest) on April 13, 2016

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Mercy Atieno (Guest) on March 25, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Anna Kibwana (Guest) on March 19, 2016

Rehema hushinda hukumu

Benjamin Masanja (Guest) on March 11, 2016

Mungu akubariki!

Grace Majaliwa (Guest) on November 1, 2015

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Charles Mrope (Guest) on July 3, 2015

Mwamini Bwana; anajua njia

Grace Mligo (Guest) on May 31, 2015

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Nancy Kabura (Guest) on May 19, 2015

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Mary Mrope (Guest) on May 16, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Mary Mrope (Guest) on April 23, 2015

Amina

Related Posts

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

SALA YA KUTUBU

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukiz... Read More

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo ... Read More

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida... Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

Kanuni ya imani

Kanuni ya imani

Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi,/ mwumba mbingu na dunia./ Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

Kuweka nia njema

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo n... Read More