Updated at: 2024-05-27 07:11:46 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kutubu ndio njia pekee ya kumrudia Mungu. Toba ya kweli ndiyo iletayo maondoleo ya dhambi. Ukiondolewa dhambi unaimarishwa na kufanywa mya. Tubu usamehewe na kufanywa mpya.
Updated at: 2024-05-27 07:12:01 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Sala za kila siku katika maisha ndiyo hazina kubwa na msaada hasa wakati wa kufa. Adumuye katika sala Mungu hatomwacha saa ya mwisho. Tusali, tusali, tusali daima…
Updated at: 2024-05-27 07:11:36 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Hakuna Binadamu anayemchukia Mungu kama hajichukii yeye mwenyewe na wale wanaomzunguka. Huwezi kusema humtaki Mungu kama hujichukii mwenyewe na wale waliokuzunguka vivyo hivyo huwezi kusema Unampenda Mungu kama hupendi wengine waliokuzunguka.
Updated at: 2024-05-27 07:11:33 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kila jambo lina Mkono wa Mungu juu yake hata kama limefanyika bila kupangwa au kukusudiwa. Mbele ya Mungu hakuna kitu kinachofanyika kwa Ajali au bahati mbaya.
Updated at: 2024-05-27 07:12:01 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kama mtu anasali kila siku katika maisha yake hakuna kitu kitakachokuwa kigumu. Sala ni njia ya kujipatia neema za kuendesha maisha yetu. Usiache kusali kila siku hata kama upo katika hali gani.
Updated at: 2024-05-27 07:11:52 (1 year ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kukosa hata mara moja inahesabika ni kukosea mbele ya Mungu. Kwa kuwa kwa Mungu hakuna kusema, 'Kukosea mara moja sio kosa bali kurudia kosa ndio kosa'. Mbele ya Mungu kila kosa lina uzito wake haijalishi ni kosa la mara ya kwanza.